Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»WALIOSHIKWA MKONO NA NABII MKUU GEOR DAVIE WAMSHUKURU WAMO VIONGOZI WA SERIKALI

    WALIOSHIKWA MKONO NA NABII MKUU GEOR DAVIE WAMSHUKURU WAMO VIONGOZI WA SERIKALI

    0
    By arushatv on November 10, 2022 Habari

    Na Geofrey  Stephen  Arusha

    Kiongozi mkuu wa huduma ya Ngurumo ya upako yenye makao makuu jijini Arusha,Dkt Nabii Geor Davie ameendelea kuwa baraka kwa wahitaji wenye mahitaji ya kimwili pamoja na kiroho kwa kuwapa mitaji

    Aidha Nabii Dkt Geor Davie amekuwa mwangaza hata kwa taasisi za Serikali kwa kuwa amejijengea tabia ya kuwasaidia kwenye maitaji mbalimbali.

    Wakizungumza kwa nyakati tofauti tofauti na Mwandishi wa habari hizi waliofanikiwa kupewa mitaji na misaada kutoka Nabii Dkt Geor Davie walisema kuwa anafanya yale ambayo yameandikwa katika maandiko matakatifu

    “Baba amekuwa ni msaada mkubwa sana hasa kwa jamii ambazo zinawaitaji,ukiangalia hata upande wa wasanii nao wamepewa misaada na mpaka wengine wamepewa magari kabisa

    Wapo wasanii ambao wanamtumikoa Mungu tena kwenye mazingira magumu hawana mtu wa kuwasaidia lakini baba Dkt Geor Davie amekuwa akiwaona,mwaka jana msanii Good luck Hozbert alipewa gari,na kama haitoshi ametoa tena kwa msanii ajulikanaye kama Mkaliwao na wote tukiangalia namna ambavyo vijana hao wanamtukuza Mungu “waliongeza

    Akiongea kwenye hafla kubwa sana ambayo ilifanyika katika mji wa daudi Kisongo Arusha wiki chache zilizopita Nabii mkuu Dkt Geor Davie alisema kuwa anazidi kutokomeza umaskini

    alisema kuwa fedha ambazo amekuwa akizitoa ni kama mbegu kwa ajili ya kutokomeza umaskini

    “Jamani kuna mtu ambaye nimempa Gari na anamtukuza Mungu,tuwasaidie watu ni mbegu tunapanda na ukifanya jambo ambalo ni Jema ni utukufu”aliongeza”.

    Naye Balozi kutoka Ngurumo ya Upako Nabii Sekela ntondolo alisema kuwa ili usipitwe na baraka za Mungu ni lazima uhakikishe kuwa unafanya jambo Kwa Mungu

    Nsekela alisema kuwa fursa zipo nyingi sana lakini wakati mwingine hazionekani kwa uraisi.

    “Tunatakiwa tujifunze kutoka kwa baba yetu Nabii Dkt Geor Davie jinsi ambavyo amefanyika baraka”aliongeza

    “Tunatakiwa kukataa udhaifu wa aina yoyote Ile na tuzidishe bidii na makanisa yetu ambayo yanaitaji kujengwa”aliongeza
    Mwisho .

     

    Post Views: 67
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleIKUNGI WALIPWA FIDIA NA JESHI MILIONI 243.7
    Next Article BODI YA WAHANDISI (ERB)YAJIPANGA KUPAMBANA NA RUSHWA NA KUKUZA WELEDI

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.