Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»LATRA ARUSHA SASA NI LESENI ZA MAGARI MAKUBWA YA ABIRIA WAMILIKI WAJIPANGE

    LATRA ARUSHA SASA NI LESENI ZA MAGARI MAKUBWA YA ABIRIA WAMILIKI WAJIPANGE

    0
    By arushatv on November 18, 2022 Habari
    Na Geofrey Stephen Arusha 
    MAMLAKA ya Udhibiti ,Usafiri Ardhini (LATRA)mkoa wa Arusha imetangaza kusitisha kutoa leseni kwa magari madogo ya abiria aina ya Haice na Noar katika jiji la Arusha na kuwataka wamiliki wa magari hayo ya biashara kujipanga kwa kununua magari makubwa.
    Aidha amewataka wasafirishaji kuzingatia mwongozo wa serikali kwa kutoa tiketi mtandao kwa mfumo wa kielekitroniki na wale wanaoendelea kukaidi wajiandae kisaikolojia kuoigwa adhabu kali.
    Akiongea katika ziara ya naibu waziri wa ujenzi na uchukuzi, Atupele Mwakibete ambaye alitembelea  ofisi za mamlaka hiyo jijini hao,meneja wa Latra Mkoa wa Arusha,Amani Mwakalebela alisema kuwa mamlaka hiyo imesitisha kutoa leseni kwa magari madogo ya abiria kutokana  na magari hayo  kutokuwa rafiki na hadhi ya jiji.
    Alisema kuwa Latra imeweka mpango mzuri wa usafiri na usafirishaji kwa kuyaondoa taratibu magari madogo aina ya haice ili kuruhusu usajiri wa magari makubwa yatajayoendana na hadhi ya jiji kwa kuwa mji umekuwa.
    “Tumesitisha kutoa leseni kwa magari aina ya Haice kutoa huduma katikati ya jiji kwa kuzingatia mahitaji ya jiji “
    Aliwataka wafanyabiashara wa magari ya abiria kununua magari makubwa yenye uwezo wa kupakia abiria wengi na yatapewa leseni ya kusafirisha abiria umbali wowote.
    Akizungumzia magari aina ya Noar yanayosafirisha abiria kwenda wilaya ya Karatu na Namanga alisema kuwa Latra imesitisha kutoa leseni ya magari hayo ila iliruhusu baadhi ya magari aina ya Noar ambayo tayari yalikuwa yameshafika nanyakitoa huduma ya usafirishaji kabla ya kusitisha zoezi la utoaji wa leseni .
    Akizungumza katika ziara hiyo naibu waziri Mwakibete aliipongea Latra kwa utendaji kazi na kuwataka kuhakikisha wanasimamia sheria ikiwemo kusomiliza changamoto za wasafiri na wasafirishanj.
    Aidha alitoa rai kwa Latra mkoani hapa kuhakikisha inatoa elimu zaidi katika sekta ya usafirishaji jambo litakalosaidia kuondoa malalamiko yasiyo na tija
    Post Views: 211
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMWINJILISTI WA KANISA LA MATAIFA YOTE APATA MAONO LENGAI OLE SABAYA KUACHIWA HURU ATAKUA KIONGOZI TENA
    Next Article WATOTO WA KIKE ZAIDI YA 7000 KUNUFAIKA NA MRADI WA UWEZESHAJI UJUZI

    Related Posts

    Tanzania na India kuendeleza Uhusiano wa Kibiashara na Uwekezaji

    March 27, 2023

    TANZANIA YAKABILIWA NA UHABA WA MABAHARIA VIJANA.

    March 27, 2023

    Marcas Ajitosa kuwania U NEC Arusha

    March 25, 2023

    VIKUNDI 47 KUPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOITA MONDULI

    March 24, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.