Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Health»WANANCHI WAFUKUZA DAKTARI KISA ULEVI NA MAJIBU MABOVU

    WANANCHI WAFUKUZA DAKTARI KISA ULEVI NA MAJIBU MABOVU

    0
    By arushatv on October 11, 2022 Health

    Njombe

    Wananchi wa kijiji cha Igombola kata ya Lupembe wilayani Njombe wameomba serikali kupitia Mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa kuondoka na mganga wa zahanati ya kijiji hicho wakimtuhumu kukosa nidhamu,ulevi pamoja na kushindwa kutibu wagonjwa mpaka watoe fedha za matibabu wakiwemo wazee.

    Katika mkutano wa hadhara wa Mkuu wa wilaya hiyo wakati akisikiliza kero pamoja na kukagua miradi ya maendeleo,wananchi wamedai kuwa daktari Samweli Tupa amekuwa na changamoto zinazopelekea vifo kwa wagonjwa hali inayowafanya kuwa na wasi wasi mkubwa wa maisha yao ndio maana wamefikia hatua ya kuomba aondolewe

    Mkuu wa wilaya ya Njombe Kissa Kasongwa mara baada ya kusikiliza changamoto hiyo ametoa maelekezo kwa mganga mkuu wa halmashauri hiyo Dkt,Suke Magembe kumuondoa daktari huyo mara moja huku mganga Mkuu wa halmashauri akikili kuwa tayari wamekwishachukua hatua za kumuondoa mtumishi huyo na kumrudisha makao makuu.

    “Maelekezo yangu,kama mtumishi huyu ana barua leo uondoke naye ili isiendelee kuwa kero,lakini mtu kama huyu ambaye ana tabia mbovu na kukiuka maadili ya kazi kumuamisha sio adhabu sasa ili tusimuonee mtu afunguliwe mashtaka kwa mujibu wa sheria za utumishi ili kama habadiriki atupishe aachie wengine wanyenyekevu kwasababu tutampeleka tena sehemu nyingine wananchi tena wanamkataa”amesema Kissa Kasongwa

    Post Views: 210
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleWANANCHI WENGI WAOMBA ELIMU KUHUSU MADINI KUTOLEWA MASHULENI
    Next Article TANZANIA KUPOKEA MKOPO WA TRILION 4.9 MAGAZETI YA LEO ARUSHA24TV

    Related Posts

    MIAKA 5, YA MREMBO MASIPETII MSICHANA MDOGO ALIYEJITOLEA KUSAIDIA JAMII NA KUACHA KAZI, ANAMILIKI NYUMBA YA MILLION 280

    March 11, 2023

    DKT MOLLEL ATOA MAJIBU MALALAMIKO UBOVU WA CHF.

    February 23, 2023

    APOTEZA MAISHA KWA KUCHAPWA FIMBO 70 ZA KIMASAI ! KOSA LA KUMTUKANA MAMA YAKE MZAZI MATUSI YA NGUONI

    January 10, 2023

    DC RUNYANGO VIJANA MJITAMBUE KATIKA AFYA NDIO MAISHA ,MJIKINGE NA MAAMBUKIZI

    December 12, 2022

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.