Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Makala»PROFESA KIKULA AAINISHA MIKAKATI YA TUME YA MADINI KWENYE UBORESHAJI WA SEKTA YA MADINI

    PROFESA KIKULA AAINISHA MIKAKATI YA TUME YA MADINI KWENYE UBORESHAJI WA SEKTA YA MADINI

    0
    By arushatv on October 13, 2022 Makala

    Na Mwandishi wa A24Tv

    Mwenyekiti wa Tume ya Madini, Profesa Idris Kikula amesema kuwa Serikali kupitia Tume ya Madini imeweka mikakati mbalimbali ya kuhakikisha Sekta ya Madini inanufaisha kila mwananchi na kuinua sekta nyingine za kiuchumi na uchumi kuendelea kukua kwa kasi.

    Profesa Kikula ameyasema hayo leo Oktoba 13, 2022 jijini Mwanza kwenye kikao cha nne cha Baraza la Wafanyakazi kilichoshirikisha Kamishna wa Tume ya Madini, Janet Lekashingo, Katibu Mtendaji wa Tume ya Madini, Mhandisi Yahya Samamba, Katibu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Nsubisi Mwasandende, Mwakilishi wa Kamishna wa Kazi – Ofisi ya Waziri Mkuu, Goodluck Luginga, watendaji kutoka Tume ya Madini Makao Makuu na kutoka Ofisi za Maafisa Madini Wakazi wa Mikoa chenye lengo la kujadili na kutatua changamoto katika utendaji kazi wa Tume ya Madini.

    Amesema kuwa mikakati iliyowekwa ni pamoja na ushirikishwaji wa watanzania katika Sekta ya Madini kupewa kipaumbele ambapo kwa sasa wananchi wameanza kutoa huduma kwenye migodi ya madini iliyoanzishwa nchini na kujipatia kipato, uboreshaji wa miundombinu na huduma nyingine za jamii ili kuweka mazingira mazuri ya kufanya biashara na kupata kipato ambacho ni endelevu hata mara baada ya kumalizika kwa shughuli za uchimbaji wa madini.

    Ameongeza kuwa mikakati mingine iliyowekwa sambamba na ukusanyaji wa maduhuli ni pamoja na kuhakikisha Sekta ya Madini inakuwa na mchango wa asilimia 10 kwenye Pato la Taifa ifikapo mwaka 2025.

    Katika hatua nyingine, Profesa Kikula amesema kuwa Tume ya Madini itaendelea kutatua changamoto zinazowakabili watumishi wake kwenye utendaji kazi na kuwataka kuendelea kuchapa kazi kwa bidii na weledi na kukidhi matarajio ya wananchi hususan wachimbaji, wachenjuaji na wafanyabiashara wa madini.

    Awali akieleza mafanikio yaliyopatikana tangu kuanzishwa kwa Tume, Profesa Kikula ameeleza kuwa ni pamoja na kuimarika kwa ukusanyaji wa maduhuli kutoka shilingi bilioni 346.78 kwa kipindi cha mwaka 2018-2019 hadi kufikia shilingi bilioni 624.61 kwa kipindi cha mwaka wa fedha 2021-2022 ikiwa ni sawa na asilimia 96.09 ya lengo la mwaka husika.

    Profesa Kikula ameendelea kueleza mafanikio mengine kuwa ni pamoja na uanzishwaji wa masoko 42 na vituo vya ununuzi wa madini 83 na ongezeko la utoaji wa leseni za madini ambapo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021-2022 Tume ilitoa jumla ya leseni za madini 9,498 ikilinganishwa na leseni 6,314 zilizotolewa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2020-2021.

    Aidha, Profesa Kikula amesema kuwa ili kusogeza huduma karibu zaidi na wadau wa madini, Tume ilianzisha ofisi mpya za madini katika mikoa ya Mbogwe na Mahenge.

    Ameendelea kusema kuwa mchango wa Sekta ya Madini kwenye Pato la Taifa umeendelea kukua kutoka asilimia 4.8 katika kipindi cha mwaka 2018 hadi kufikia asilimia 7.2 katika kipindi cha mwaka 2021.

    Post Views: 97
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleUNYAMA MWANAMKE AKATWA SEHEMU ZA SIRI ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV
    Next Article RAIS SAMIA ASHAURIWA KUKUTANA NA WADAU WA SEKTA YA MADINI NCHINI.

    Related Posts

    ASKOFU MASANGWA AKOSHWA NA MCHUNGAJI ALIYETUMIKIA KANISA KWA MIAKA34 AMEACHA ALAMA KUBWA

    February 26, 2023

    MZEE MOLLEL AZIKWA KIJIJINI KWAKE WANANCHI WAMWAGA MACHOZI WAZMIA WAKIAGA MWILI WAKE

    February 7, 2023

    WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezindua zoezi la ugawaji wa vishikwambi 293400 Kwa walimu wote nchini

    November 5, 2022

    WANANCHI WENGI WAOMBA ELIMU KUHUSU MADINI KUTOLEWA MASHULENI

    October 11, 2022

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.