Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Health»MILIONI, 500 ZAKAMILISHA KITUO CHA AFYA WANACHI WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    MILIONI, 500 ZAKAMILISHA KITUO CHA AFYA WANACHI WAMSHUKURU RAIS SAMIA

    0
    By arushatv on October 27, 2022 Health

    Na John Mhala,Bumbuli

    Nyumba tano za Upanuzi wa Mradi wa Kituo cha Afya kata ya Mgwashi Jimbo la Bumbuli Wilayani Lushoto Mkoani Tanga umegharimu zaidi ya shilingi milioni 247.6 hadi sasa

    Nyumba hizo ni pamoja na jengo la Maabara,jengo la Mochwari,jengo la Upasuaji,jengo la Wazazi na nyumba ya Mtumishi ujenzi wa nyumba hizo umefikia hatua ya asilimia 80 kukamilika.

     

    Mganga Mfawidhi wa Kituo cha Afya Mgwashi,Kelvin Shukia alisema mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Lushoto ,Kalist Lazaro aliyetembelea mradi huo kuwa mradi ulikuwa ukamilike ndasni ya siku 90 ambapo ulikuwa ukamilike julai mosi mwaka huu.

    Alisema lakini hadi sasa mradi huo haujakamilika kutokana na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji wake na amemwomba Mkuu wa Wilaya kuhakikisha anafuatilia changamoto hizo miradi hiyo inakamilika kwa faida ya wananchi.

    Mganga huyo alisema wananchi walijitoa katika kusaidia ujenzi wa miradi hiyo ikiwa ni pamoja na kuchimba misingi na uandaaji wa viwanja kwa ajili ya ujenzi wa majengo hayo matano.

    Alisema ili majengo hayo yaweze kukamilika zaidi ya shilingi milioni 252 zinahitajika na ameiomba serikali kukumbuka kupeleka fedha kwa ajili ya miradi hiyo ili wananchi waweze kupata huduma.

    Mkuu wa Wilaya aliwahakikishia wananchi wa Mgwashi kuwa serikali haiataweza kuwaacha katika kumalizia majengo hayo na suala hilo atalivalia njuga na kuhakikisha fedha zinakwenda na kumalizia ujenzi wa majengo hayo.

    Lazaro alisema ujenzi wa Kituo cha Afya Mgwashi ni mkombozi kwa wananchi 180,000 kwa sense ya mwaka 2012 waliopo katika kata hiyo na jimbo la Bumbuli kwa kuwa itawaondolea adha ya kuenda umbali mrefu kusaka huduma ya afya.

    Alisema changamoto zote zilizoelezwa na Mganga Mfawidhi wa Kituo hicho cha Afya zitafanyiwa kazi na kila kitu kitakwenda sawa kwani serikali ya Rais Samia Suluhu Hassan iko kwa ajili ya wananchi.

    Mwisho

    Post Views: 75
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleTUZO ZA UBORA ZA KITAIFA 2022/2023 KUZINDULIWA RASMI LEO.
    Next Article MBATIA AMBURUZA MAHAKAMANI SELASINI KULIPWA MABILIONI ,MAGAZETI YA LEO ARUSHA 24TV

    Related Posts

    MIAKA 5, YA MREMBO MASIPETII MSICHANA MDOGO ALIYEJITOLEA KUSAIDIA JAMII NA KUACHA KAZI, ANAMILIKI NYUMBA YA MILLION 280

    March 11, 2023

    DKT MOLLEL ATOA MAJIBU MALALAMIKO UBOVU WA CHF.

    February 23, 2023

    APOTEZA MAISHA KWA KUCHAPWA FIMBO 70 ZA KIMASAI ! KOSA LA KUMTUKANA MAMA YAKE MZAZI MATUSI YA NGUONI

    January 10, 2023

    DC RUNYANGO VIJANA MJITAMBUE KATIKA AFYA NDIO MAISHA ,MJIKINGE NA MAAMBUKIZI

    December 12, 2022

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.