Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»Mtakwimu mkuu asema sensa imeingiza Tanzania kwenye rekodi za kidunia

    Mtakwimu mkuu asema sensa imeingiza Tanzania kwenye rekodi za kidunia

    0
    By arushatv on September 15, 2022 Habari
    MTAKWIMU mkuu wa Sensa ya watu na makazi nchini ameipongeza taasisi ya dini ya kiislamu ya Twarika Qadiriya, viongozi wa mila na dini mkoani Arusha kwa kuipa heshina serikali kwa kufanikisha kuhamasisha wananchi kushiriki zoezi hilo na kuifanya  Tanzania kuingia kwenye rekodi ya kidunia.
    Akisoma taarifa kwa niaba ya mtakwimu mkuu wa serikali,katika hafla ya kumpongez rais Samia Suluhu Hasan kwa kuandaa na kufanikisha zoezi hilo,Seif Kuchengo alisema kuwa taaisis hiyo ya dini ilikuwa mstari wa mbele katika kuratibu na kuyashirikisha makundi mbalimbali katika kuhamasisha zoezi la sensa hapa nchini.
    Alisema kuwa ofisi ya mtakwimu  mkuu wa serikali haina budi kupongeza taasisi zote zilizoshiriki kufanikisha zoezi hilo ambalo ni sensa ya sita  hapa Tanzania.
    Uhamasishaji uliofanywa na viongozi wa dini,wanasiasa ,viongozi wa wilaya na mkoa  hapa nchini umefanikisha Tanzania kuingia kwenye rekodi ya kidunia na kuwataka viongozi hao kuendelea na moyo huo wa kuunga mkoano kwenye masuala mengine ya maendeleo.
    Alisema kwa kufanikisha zoezi hilo nchi yetu imekuwa miongozi mwa nchi za Afrika na dunia zilizofanya sensa ndani ya mzunguko wa miaka 2020 ,mzunguko ambao unazitaka nchi kufanya sensa ndani ya miaka 10 kuanzia mwaka 2015 hadi mwaka 2024.Hivyo Tanzania imeingia kwenye  rekodi hiyo.
    Awali kiongozi wa Twarika mkoa wa Arusha,Sheikh Haruna Husein alimshukuru  rais Samia Suluhu hasani kwa kuandaa na kufanikisha zoezi la Sensa ya watu na makazi hapa nchini jambo ambalo litasaidia kuipa fursa serikali kuwaletea maendeleo  ya dhati wananchi wake.
    Aidha sheikh Haruna pamoja na kuwashukuru viongozi wa dini mbalimbali makundi ya mama Ntilie,Bodaboda ,viongozi wa mila Laigwanan na washiri,wanasiasa na viongozi wa ngazi ya wilaya na mkoa alisema ipo haja ya kuendeleza mshikamano huo katika kuunga mkono juhudi za serikali katika kupambana na umasikini.
    Akiongea kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha,John Mongela, Leokadia Mtei ambaye ni mtakwimu mkuu mkoa wa Arusha, aliwashukuru wananchi wa mkoa wa Arusha kwa kufanikisha zoezi  hilo ambapo kwa Arusha wamefanikiwa kuandikisha watu na makazi kwa kiwango kikubwa na hivyo kuvuka malengo waliojiwekea.
    Aliwataka wananchi kusubiri Takwimu halisi zitakazotolewa na serikali ambazo zitatangazwa na rais ili serikali iweze kupanga mikakati ya kuwaletea maendeleo yatakayowanufaisha wananchi .
    Ends.
    Post Views: 326
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleWananchi Monduli waomba uzio kulinda vyanzo vya maji.
    Next Article PANYA RODI TISHIO POLISI WAMWAGWA KILA KONA DAR , MAGAZETI YA LEO NA A24TV

    Related Posts

    Kamati yapitisha makadirio ya matumizi na maendeleo 2023/2024 kwa Wizara Uwekezaji Viwanda na Biashara.

    March 23, 2023

    MWANDISHI WA HABARI MAARUFU ALLAN ISACK AITAKA NAFASI YA MNEC

    March 23, 2023

    Vyombo vya Dola na wanasheria kushirikiana kutokomeza ujangili Babati

    March 22, 2023

    JIJI LA ARUSHA LATOA MIKOPO YA SHILINGI BILION 2.6 KWA VIJANA WENYE MAITAJI MAALUM NA WANAWEKE

    March 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.