Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»THIBITINI UBORA BADALA YA KUDHIBITI BUNIFU – PROF MDOE

    THIBITINI UBORA BADALA YA KUDHIBITI BUNIFU – PROF MDOE

    0
    By arushatv on June 21, 2022 Habari

    Na WyEST,

    DODOMA.

    Taasisi na Mamlaka za Uthibiti ubora wa bidhaa na huduma zimeshauriwa kuangalia upya sheria wanazozitumia ili kuhamasisha ubunifu na kulinda wabunifu wachanga.

    Ushauri huo umetolewa Jijini Dodoma na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Prof. James Mdoe wakati akifungua kikaokazi cha kupitia Mwongozo wa Kitaifa wa Kuibua, Kutambua na Kuendeleza Ugunduzi, Ubunifu na Maarifa Asilia wa Mwaka 2018.

    Prof. Mdoe amesema kazi za taasisi hizo ni kuthibiti ubora kwa maana ya kuhakikisha huduma na bidhaa zinazozalishwa zinakuwa na ubora unaotakiwa ikiwa ni pamoja na kusaidia wabunifu wachanga kufikia ubora na viwango vinavyotakiwa ili bunifu zinazobuniwa ziweze kumsaidia mbunifu mwenyewe, jamii na Taifa.

    “Ujumbe wangu ninaoupeleka kwa Regulators tena leo nafahamu kwa asili ya sheria zilizounda taasisi hizi za Uthibiti ubora zimekaa kipolisipolisi na hazihamasishi ubunifu kwa hiyo kama mtu akija na kitu chake amekibuni yaani kitu cha kwanza anaulizwa una leseni? Umelipia?” amefafanua Prof. Mdoe.

    Prof. Mdoe amesema wabunifu wachanga wanatakiwa kupewa miongozo ya namna bora ya kuboresha bunifu zao ili kufikia viwango vya ubora vya bidhaa na huduma hivyo taasisi husika zina wajibu wa kuondoa changamoto zinazowakabili.

    “Wabunifu hawa ili waweze kufika malengo yao wanahitajika kushikwa mkono, changamoto zinaweza kumkatisha tamaa na kuamua kuacha kuendelea na shughuli za kiubunifu,” amebainisha Prof. Mdoe.

    Aidha, amesema Mwongozo huo unaopitiwa una lengo la kumwezesha mbunifu kuanza kunufaika mwenyewe, jamii na taifa, ambapo mpaka sasa umewezesha kuibuliwa kwa wabunifu wapatao 2,647 kupitia Mashindano ya Kitaifa ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu (MAKISATU).

    Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Idara ya Sayansi, Teknolojia na Ubunifu Prof. Maulilo Kipanyula akizungumza wakati wa kumkaribisha Katibu Mkuu amesema kikao hicho kinawapa fursa wadau mbalimbali katika kuboresha Mwongozo huo ili wadau waweze kuutumia na kuongeza hamasa ya kuibua na kuendeleza wabunifu wa ngazi ya chini.

    “Mkutano huu unajumuisha Wizara,Taasisi za Umma na hata zile za binafsi nazo tumeita wawakilishi ili tutajadili na kutengeneza huu Mwongozo ili kuchochea ubunifu,” amesema Prof. Kipanyula.

    Naye Afisa Viwango kutoka Shirika la Viwango Tanzania (TBS) Mathias Nyaisanga amesema shirika hilo lipo kusaidia wabunifu kushindana katika soko la ndani na nje ya nchi.

    Bw. Nyaisanga amebainisha kwamba kupitia uthibiti wa ubora wa bidhaa Shirika hilo linawasaidia wabunifu wachanga na wakubwa kufikia viwango na ubora wa bidhaa wanazozalisha.

    Post Views: 87
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleALIYEKUA MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA PIMA NA WENZAKE WASOMEWA MASHTAKA MAPYA 6
    Next Article SAKATA LA LOLIONDO MABALOZI WATETEA MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV

    Related Posts

    Tanzania na India kuendeleza Uhusiano wa Kibiashara na Uwekezaji

    March 27, 2023

    TANZANIA YAKABILIWA NA UHABA WA MABAHARIA VIJANA.

    March 27, 2023

    Marcas Ajitosa kuwania U NEC Arusha

    March 25, 2023

    VIKUNDI 47 KUPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOITA MONDULI

    March 24, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.