Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»WIKI YA HUDUMA YA FEDHA KITAIFA KUFANYIKA JIJINI MWANZA NOVEMBA 21MPAKA 26 MWAKA HUU.

    WIKI YA HUDUMA YA FEDHA KITAIFA KUFANYIKA JIJINI MWANZA NOVEMBA 21MPAKA 26 MWAKA HUU.

    0
    By arushatv on November 16, 2022 Habari

    Na Doreen Aloyce, Dodoma

    Katika kuelekea wiki ya huduma ya fedha inayotarajia kufanyika Novemba 21 mpaka 26 Jijini Mwanza mwaka huu, Wizara ya Fedha imejipanga kujenga uelewa na weledi kwa Umma juu ya uelewa wa fedha ambapo imesema mpaka sasa asilimia 40 ya idadi ya watanzania waishio vijijini hawajafikiwa

    Aidha katika utekelezaji wa Program ya utoaji Elimu wa masuala ya Fedha Serikali inakusudia ifikapo mwaka 2025 takribani asilimia 80 ya wananchi watakuwa wamepata uelewa wa masuala ya Fedha.
    Akizungumza Jijini Dodoma alipokuwa akitoa maelekezo kuhusu wiki ya huduma ya Fedha kitaifa Kamishna uendeshaji wa sekta ya Fedha Charles Mwamwaja kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara alisema kuwa Kutokana na Utafiti wa FinScop wa mwaka 2017 Nchini ni asilimia 48.6 tu ya nguvu kazi ndiyo waliotumia huduma rasmi za fedha na hivyo kubaki na kundi kubwa la watanzania ambao hawafaidiki na huduma hizo.

    “Hivyo kukosa fursa za kuboresha maisha yao kupitia shughuli mbalimbali za kiuchumi na hatimaye kuchangia katika kukuza Pato la Taifa,”alisema.

    Aidha alieleza kuwa malengo ya wiki ya huduma za fedha ni pamoja na kujenga uelewa na weledi kwa umma katika matumizi sahihi ya huduma za fedha zinazotolewa ili kujenga uchumi na kuondoa umaskini.

    Na Kuimarisha ufanisi wa masoko ya Fedha kupitia elimu ya Fedha,kuongeza upatikanaji wa huduma za fedha,kutoa elimu ya kuwezesha kumlinda mtumiaji wa huduma za kifedha,kuwezesha wananchi kusimamia vizuri Rasilimali fedha.

    “Kuwezesha wajasiriamali wadogo kuongeza ujuzi na matumizi sahihi ya huduma za fedha katika kukuza biashara zao,kuimarika kwa Utamaduni wa kujiwekea akiba,kukopa na kulipa madeni pamoja na kuongezeka kwa mchango wa sekta ya Fedha kwenye ukuaji wa uchimi,”alisema.

    Aidha alisema kuwa wiki ya huduma za fedha inalenga kuwafikia wadau mbalimbali wakiwemo watumishi wa umma, wanafunzi,wakufunzi,wanawake,vijana,watu wenye mahitaji maalum,wajasiriamali wadogo na wakati(SMEs),asasi za kiraia,wahariri na waandishi wa vyombo vya habari,watoa huduma za fedha,watoto na ummakwa ujumla.

    Maadhimisho ya wiki ya huduma za fedha kitaifa ni utekelezaji wa Mpango mkuu wa mendeleo ya sekta ya Fedha wa mwaka 2020/21-2029/30,elimu kwa umma ni moja ya maeneo ya kipaumbele katika utekelezaji wa Mpango huo.

    Wizara ya fedha na Mpango imeandaa programu ya kutoa elimu kwa umma ya mwaka 2021/22-2025/26 programu hiyo imeweka mikakati ikiwa ni pamoja na matukio na mbinu mbalimbali zitakazotumika katika utoaji wa elimu ya Fedha kwa umma.

    Mwisho.

    Post Views: 75
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMGAO WA MAJI PASUA KICHWA ? KOCHA WA SIMBA ANASWA NA DAWA ZA KULEVYA ,MAGAZETI YA LEO ARUSHA24TV
    Next Article BISKUTI ZA BANGI TISHIO JIPYA KWA WANAFUNZI WA VYUO ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV .

    Related Posts

    Tanzania na India kuendeleza Uhusiano wa Kibiashara na Uwekezaji

    March 27, 2023

    TANZANIA YAKABILIWA NA UHABA WA MABAHARIA VIJANA.

    March 27, 2023

    Marcas Ajitosa kuwania U NEC Arusha

    March 25, 2023

    VIKUNDI 47 KUPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOITA MONDULI

    March 24, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.