Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Elimu»WAANDISHI ANDIKENI HABARI BUNIFU ZINAZOCHOCHEA UKUAJI WA UCHUMI

    WAANDISHI ANDIKENI HABARI BUNIFU ZINAZOCHOCHEA UKUAJI WA UCHUMI

    0
    By arushatv on November 4, 2022 Elimu

     NA: VERONICA MAKONGO, ARUSHA

    Waandishi wa habari nchini wametakiwa kuandika habari zenye manufaa Kwa jamii Kwa kuandika habari bunifu zinazolenga kuwakwamua wananchi  kuondokana janga la umaskini.

    Sekta ya habari na utangazaji ikitumika ipasavyo hususani vyombo vya habari mtandaoni kwa kuzingatia ukuaji wa teknolojia  vinaharakisha  zoezi la kuipasha jamii habari kwa wepesi na haraka  zaidi hivyo kuwa chachu ya mabadiliko

    Mkurugenzi wa taasisi ya wanahabari ya MAIPAC  Bw Musa Juma akitoa hotuba katika mahafali ya 16 ya chuo cha uandishi wa habari Fanikiwa. PICHA na Marystela Bryson.

    Hayo yameelezwa na Mkurugenzi mtendaji wa taasisi ya wanahabari inayosaidia jamii za pembezoni nchini MAIPAC, Bw Musa Juma wakati akihutubia wahitimu na wazazi katika mahafali ya 16 ya Chuo cha Uandishi wa Habari na Utangazaji Fanikiwa Arusha yaliyofanyika katika ukumbi wa PPS  jijini Arusha mapema leo.

    Mkurugenzi huyo amesema kuwa ulimwengu wa sasa umekuwa, haswa  katika eneo la sayansi na teknolojia hvyo wana habari wanapaswa kukimbia na ukuaji huo wa teknolojia kwa kuandika habari Bora na bunifu pia kuanzisha vyombo vya habari vya mitandaoni ambavyo  vitawasaidia wao kujiajiri.

    Wahitimu Wa Chuo Cha Uandishi wa Habari na Utangazazji Fanikiwa Ausha. PICHA na Marystela Bryson

    Hata hivyo ameeleza kuwa  waandishi wengi wanaweza kufungua “Blog, radio mtandao na  Tv za Mitandaoni ambazo  wanaweza kupeleka maudhui mbali mbali ya kihabari na kupitia vyombo hvyo watapatikana wawekezaji mbalimbali ambao wataweka matangazo ya biashara zao ili zionekane na watazamaji au pengine wasomaji.Musa Juma ambaye pia ni Mjumbe wa Bodi MISA – TAN na Mkuu wa magazeti ya mwananchii Mkoani Arusha amewataka wahitimu hao wa ngazi ya Stashahada kuzingatia maadili wawapo kazini lakini pia kuwa wabunifu katika kuandika habari za mazingira, kilimo, uchumi, na  mabadiliko ya TABIA NCHI ili kusaidia kuwaweka katika mazingira mazuri zaidi ya kihabari.

    Naye mkuu wa chuo hicho Bwana Andrea Ngobole, amewataka wazazi  wa wahitimu hao  kuwaendeleza zaidi vijana hao katika chuo kikuu ili waendelee kupata elimu zaidi juu ya tasnia ya habari na sekta nyinginezo.

    Mkuu wa Chuo cha uandishi wa habari na Utangazaji Fanikiwa Bw Andrea Ngobole akitoa hotuba kwa wahitimu wa chuo hicho mapema leo. PICHA NA Marystela Bryson.

    Aidha katika Mahafali Hayo wahitimu wapatao 40 wamehitimu mafunzo yao ya umahiri katika Tasnia ya habari na utangazaji ambapo pia wamedhamiria kwenda kuleta mabadiliko makubwa katika sekta ya habari na utangazaji.

    Wahitimu wakiwa katika picha ya pamoja wakisikiliza Kwa makini hotuba ya mhgeni rasmi.

     

     

     

     

     

    Post Views: 78
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleBILIONI 2.3 KUKAMILISHA UJENZI WA BWENI LA KIKE MAENDELEO YA JAMII
    Next Article MBUNGE WA CHADEMA AMVAA MNYIKA MAHAKAMANI ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV

    Related Posts

    SHULE YA BILIONEA SANINIU LAIZER YAPATA UFADHILI MZITO WA MADAWATI NA MEZA ZA KISASA

    March 13, 2023

    Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Carolyne Nombo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa umahiri.mkubwa

    February 28, 2023

    WIZARA YA ELIMU YATOA UFAFANUZI WALIO FUTIWA MATOKEO YA MITHIANI WA KIDATO CHA NNE

    February 9, 2023

    WANAFUNZI 170 WAPATIWA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KUTOKA OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA MONDULI.

    January 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.