Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»Halmashauri ya Arusha yamkabithi cheti cha shukrani  mfanyabiashara maarufu Monaban

    Halmashauri ya Arusha yamkabithi cheti cha shukrani  mfanyabiashara maarufu Monaban

    0
    By arushatv on August 11, 2022 Habari
    Na Geofrey Stephen ,Arusha
    Arusha.Halmashauri ya Arusha  kupitia baraza la madiwani wamemkabithi mfanyabiashara maarufu Dk Philemon Mollel (Monaban) cheti  cha  shukrani kwa kuchangia mifuko 60 ya saruji kwa ajili ukarabati wa  madarasa shule ya sekondari Oldadai katika halmashauri ya Arusha.
    Akikabithi cheti hicho leo jijini Arusha katika baraza  hilo, Mkurugenzi wa  halmashauri ya Arusha   ,Suleman Msumi  amesema kuwa, wamefikia  hatua  ya kukabithi cheti  hicho kutokana na mchango mkubwa alionao katika shughuli mbalimbali za  maendeleo .
    Amesema kuwa,walikuwa na zoezi la kitaifa  ambalo hufanyika  kila  mwaka la mwenge  wa uhuru kwa ajili ya kuweka  jiwe  la msingi na  kuzindua  baadhi ya miradi  ya halmashauri hiyo  iliyofanyika  julai  mwaka  huu.
    “Tuliweza kushirikisha wadau  mbalimbali kuhusiana na swala letu  ambapo  Dk Philemon alifanikiwa kutupatia mifuko 60 ya saruji  kwa ajili ya kumalizia shule  ya sekondari Oldadai,na hivyo  kwa  kutambua  mchango  wake  tukaona ni  busara  kwa  halmashauri  kumkabithi  cheti  cha shukrani.”amesema Msumi.
    Kwa upande wake,Mfanyabiashara huyo  Dk  Philemon Mollel ameshukuru sana baraza hilo kwa kutambua mchango wake  na kukumbuka  fadhila  kwa kumkabithi  cheti  cha shukrani jambo ambalo  linatoa  motisha wa  kuendelea kusaidia zaidi. 
    Dk.Mollel amesema kuwa,kitendo kilichofanywa na halmashauri  hiyo  ni  jambo kubwa sana na linahitaji  kuigwa na taasisi zingine ili  watu  waendelee kuwa na motisha  wa kuisaidia  jamii  katika maswala  mbalimbali.
    “Mimi niseme tu  nimefurahishwa sana kwa zoezi  hili  na kipekee naahidi kuendelea  kusaidia zaidi katika maswala  mbalimbali ya maendeleo  ili  jamii yetu  iweze kusonga mbele na kuondokana na changamoto mbalimbali. “amesema Mollel.
    Mwisho.
    Post Views: 302
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleRAILA NA RUTO MNYUKANO MKALI MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV
    Next Article BEI YA VYAKULA JUU WAKULIMA WALIA ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV .

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.