Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Break News»SIMANZI JIJI LA ARUSHA WATATU WAFARIKI DUNIA KWA AJALI USIKU SAA KUMI

    SIMANZI JIJI LA ARUSHA WATATU WAFARIKI DUNIA KWA AJALI USIKU SAA KUMI

    0
    By arushatv on July 13, 2022 Break News

     

    Na mwandishi wa A24Tv

    Watu watatu wa familia moja akiwemo mtoto mdogo,wakazi wa kata ya Terat katika jiji la Arusha,wamepoteza Maisha papo hapo kwa ajali baada ya kugongwa na gari wakitoka hospitalini wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki.

    Tukio hilo la kusikitisha limetokea mapema leo majira ya saa 10.45 usiku katika barabara ya bypass katika jiji la Arusha wakati marehemu wakitoka kumpeleka hospitalini, mtoto Ebenezer Mollel mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu aliyekuwa ameandikiwa sindano za masaa.

    Wengine waliofariki dunia ni pamoja na mama wa mtoto ,Neema Mollel(27) pamoja na mdogo wake ,Agustino Mollel (24) ambaye alikuwa dereva wa pikipiki .

    Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo,John Mushi marehemu hao walipoteza maisha eneo la tukio baada ya kupata majeraha makubwa na kuvuja damu nyingi.

    Alisema walishuhudia miili ya marehemu hao wakiwa wamevunjika na kusagika mikono na miguu huku mtoto na dereva wakipasuka kichwa na kusagika.

    Naye kaka wa marehemu Daud Mollel alisema kuwa marehemu waligongwa kwa nyuma wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki na gari ambalo halikujulikana baada ya kutosimama katika eneo la Karvati ,Terat.

    Alisema kuwa mara baada ya kupata taarifa juu ya ajali hiyo alifika eneo la tukio na kushuhudia miili ya marehemu wakiwa ikiwa na majeraha makubwa sehemu mbalimbali za miili yao.

    “Marehemu walitoka nyumbani Terat majira ya saa 10 usiku kwenda hospitali ya Murieti baada ya mtoto (marehemu)kuandikiwa sindano za masaa,wakati wakirudi majira ya saa kumi na moja kasoro ndipo walipogongwa na gari kwa nyuma na kufariki dunia”alisema

    Kamanda wa polisi Mkoa wa Arusha, Justine Masejo alithibitisha tukio hilo na kueleza kuwa bado wanafanya uchunguzi kujua chanzo cha tukio hilo.

    Kamanda alisema kuwa gari lililohusika na tukio hilo halikuweza kupatikana na polisi wanaendelea na uchunguzi ili kumtia mbaroni dereva wa gari hilo ambaye alitoweka mara baada ya ajali hiyo.

    Miili ya marehemu imehifadhiwa katika chumba cha maiti katika kituo cha afya cha Murieti kusubiri taratibu wa uchunguzi .

    Post Views: 94
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleTEAM JPM WAAPA KUSIMAMISHA MGOMBEA URAIS 2025 MAGAZETI YA LEO NA A24TV .
    Next Article DIWANI MSOFE SISI ATUWEZI KUSHIKWA MASIKIO NINAUZOEFU TUNATAKA KIKAO RASMI

    Related Posts

    MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA AMETOA MILION 33 KUNUNUA UNGA WA LISHE KWA WENYE MAHITAJI MAALUM

    February 9, 2023

    KOREA KUSINI NA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA WALETA PIKI PIKI MPYA ZA KUTUMIIA UMEME

    February 5, 2023

    BREAKING NEWS : MUSA JUMA MWENYEKITI MPYA JOWUTA SERIKALI YAAHIDI USHIRIKIANO

    January 29, 2023

    WAFANYA BIASHARA SAMUNGE JIJINI ARUSHA WAPOKEA MILLIONI 100 KUTOKA KWA NABII MKUU GEORDAVIE WAHIDI MAKUBWA KATIKA KUKUZA MITAJI YAO

    January 27, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.