Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Uncategorized»Ruwasa yaokoa bilioni 57.4 miradi ya maji fedha kwenye miradi ya maji

    Ruwasa yaokoa bilioni 57.4 miradi ya maji fedha kwenye miradi ya maji

    0
    By arushatv on July 19, 2022 Uncategorized

    Mwananchi wetu,Dodoma.

    Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Nchini Vijijini (Ruwasa) imeokoa zaidi ya Sh57.4 bilioni ambayo ilikuwa itumike kugharamia miradi ya maji vijijini.

    Fedha hizo zimeokolewa katika kipindi cha mwaka 2021/2022 katika miradi ya maji 86 ambayo ilikuwa itekelezwe kwa gharama ya Sh367.3 bilioni.

    Mkurungezi Mkuu wa Ruwasa, Clement Kivegalo amesema hayo leo Jumanne Julai 19,2022 wakati akielezea utekelezaji wa shughuli mbalimbali za taasisi na mwelekeo kwa mwaka wa fedha 2022/2023.

    “Hapo awali ujenzi wa miradi ya maji ulikuwa ukifanyika kwa gharama kubwa ukilinganishwa na uhalisia. Kwa kutambua hilo katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/2022 ilifanya majadiliano ya kina ya mikataba na wakandarasi kwa miradi 86,”amesema.

    Hata hivyo, Kivegalo amesema baada ya majadiliano na maelezo kuhusiana na miradi hiyo walitekeleza kwa Sh309.9 bilioni na hivyo kuokoa Sh57.4 bilioni ziliokolewa.

    Kuhusu bei za maji, Mkurugenzi huyo amesema Agosti mwaka huu bei za ukomo wa maji zitaanza kutumika ili kuondoa malalamiko ya bei kubwa ya maji katika baadhi ya maeneo.

    “Ruwasa itaendelea kufanya mapitio na maboresho ya bei za ukomo wa maji kila mwaka ili kuhakikisha bei za maji zinaendana na uhalisia wa gharama za uendeshaji kwa kipindi husika,”alisema.

    Mamlaka ya Maji safi na usafi wa mazingira Vijiji ilianzishwa na Serikali kutekeleza miradi ya maji vijijini na tangu imeanzishwa imefanikiaa kutekeleza miradi kadhaa ya Maji.
    Mwisho

    Post Views: 63
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMADEREVA 35 BARANI AFRIKA KUCHUANA VIKALI KATIKA MBIO ZA MAGARI ARUSHA
    Next Article RAIS SAMIA AMTEUA IGP MPYA ,KUAPISHWA LEO ! MAGAZETI YA LEO ARUSHA24TV

    Related Posts

    SHEHENA LA MBOLEA ILIYO JAZWA MCHANGA YAKAMATWA WAZIRI ATOA MAAGIZO MAZITO

    March 5, 2023

    Wadau wa Tehama mkoani Arusha watakiwa kutoa ushirikiano kuhakikisha uwepo wa kituo cha ubunifu wa Tehama.

    February 28, 2023

    KATIBU TAWALA MKOA WA ARUSHA ASISITIZA MAFUNZO KUTOKA TUME YA USHINDANI NCHINI

    February 23, 2023

    TANESCO NCHINI KUTEKELEZA MIRADI YA UZALISHAJI UMEME, KUONDOA CHANGAMOTO KWA JAMII

    February 23, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.