Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»MWENGE WAZINDUA MIRADI YA BILIONI 5.2 LUSHOTO

    MWENGE WAZINDUA MIRADI YA BILIONI 5.2 LUSHOTO

    0
    By arushatv on June 3, 2022 Habari

    Na Geofrey Stephen,Lushoto

    Miradi 18 ya Elimu,Afya,Barabara na Maji yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 5.2 imezinduliwa na mbio za mwenge katika Wilaya Lushoto yenye Halmashauri mbili za Bumbuli na Lushoto Mkoani Tanga.

    Akisoma taarifa mbele ya Kiongozi wa Mbio za Mwenge Kitaifa Sahili Geraruma ,Mkuu wa Wilaya ya Lushoto,Kalist Lazaro alisema katika Halmashauri ya Lushoto mwenge umekimbizwa Kwa km 359 na kuzindua miradi 11 yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 3.4.

    Lazaro alisema katika Halmashauri ya Bumbuli Mwenge ulizindua Miradi ya Maendeleo 7 yenye thamani ya zaidi ya Shilingi Bilioni 1.8.

    Mkuu huyo alisema Miradi yote imezingatia thamani ya pesa,Ubora wa Kiwango cha majengo na kufuata Kanuni na taratibu za manunuzi.

    Akizungumza mara bàada ya kuzindua miradi na kuweka jiwe la Msingi katika Miradi kadhaa Geraruma aliwataka watendaji wa Halmashauri kote Nchini kuhakikisha Miradi yote inazingatia thamani ya pesa na kuwa katika Ubora na kuwataka watendaji kuacha ubabaishaji na kufanya kazi Kwa mazoea hilo halitakubalika.

     

    Geraruma alisema Rais Samia Suluhu Hassani anatoa pesa Kwa ajili ya Miradi mbalimbali Nchini hivyo Watendaji wa Halmashauri isiwe sehemu ya wao kufanya mambo kiholela na kutumia pesa katika Miradi ikiwa chini ya Kiwango hilo hatalivumilia.

    Alisema na inasikitisha kuona Mtendaji idara ya Injinia aliyeisomea kazi yake na kupata elimu ya juu anafanya mambo kinyume kabisa na utaratibu na kusema kuwa watendaji wa namna hiyo wanapaswa kuachia ngazi kwa kuwa wanamkatisha tamaa Rais na hilo halitavumiliwa.

    Mwisho

     

    Post Views: 570
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleUjumbe mkuu wa kiongozi wa mbio za mwenge
    Next Article LUSHOTO YANG’ARA MIRADI YA MAJI MWENGE WAZINDUA,MBUNGE AMFAGILIA DC KALISTI USIMAMIZI MIRADI

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.