Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»Mwenge wazindua Makao makuu ya Enduimet WMA na Kituo Cha kutoa taarifa kwa watalii.

    Mwenge wazindua Makao makuu ya Enduimet WMA na Kituo Cha kutoa taarifa kwa watalii.

    0
    By arushatv on June 26, 2022 Habari

    Mwenge wazindua Makao makuu ya Enduimet WMA na Kituo Cha kutoa taarifa kwa watalii.

    Mwandishi wetu, Longido

    Mwenge wa Uhuru ,umezindua mradi wa majengo ya Makao Makuu ya Jumuiya hifadhi ya Wanyamapori ya Enduimet wilayani Longido ambao umegharimu kiasi cha sh 651.7 milioni.

    Mradi huo ambao sasa utawezesha Enduimet WMA kuwa na Kituo cha taarifa za watalii umejengwa na Taasisi ya jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF) Kwa ufadhili wa shirika la uhifadhi la kimataifa(WWF-TCO).

    Kiongozi wa mbio za mwenge Sahili Geraruma alipongeza TNRF na Enduimet WMA mwa kutelekeza mradi huo ambao unakwenda sambamba na jitihada za Serikali kukuza Utalii nchini.

    Geraruma alitaka Enduimet WMA kutunza majengo hayo ili yatumike Kwa muda mrefu zaidi kusaidia sekta ya Utalii nchini.

    Kiongozi huyo wa Mwenge alishukuru wafadhili WWF na wasimamizi na watekelezaji wa mradi Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF)Kazi nzuri ambayo wamefanya.

    Akizungumza baada ya kuzinduliwa mradi huo, Mkurugenzi wa TNRF Zakaria Faustin alishukuru Serikali Kwa kutambua mchango na jitihada zao za kuendeleza uhifadhi nchini.

    “Mradi huu ni sehemu tu ya miradi ya TNRF ambayo tunaifanya nchini katika maeneo mbalimbali ili kuendeleza uhifadhi Kwa faida ya sasa na vizazi vijavyo”amesema.

    Mwakilishi wa shirika la uhifadhi la WWF-TCO Professor Noah Sitat amesema wataendelea kufadhili miradi mingine Enduimet katika jitihada za kupunguza ujangili.

    Mwisho

    Post Views: 375
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV
    Next Article CHADEMA YASISITIZA KINA MDEE KUONDOLEWA BUNGENI MAGAZETI YA LEO NA A24TV

    Related Posts

    Maafisa Mawasiliano na Uhusiano Serikalini waaswa kutangaza mafanikio ya utekelezaji wa MKUMBI

    March 30, 2023

    SHIRIKA La Umeme Tanzania (TANESCO), limezindua Programu ya Mpango wa miaka minne wa jinsia

    March 30, 2023

    Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Dkt. Jim Yonazi ameridhishwa maendeleo ya miradi ya ujenzi inayosimamiwa na Ofisi hiyo

    March 30, 2023

    KILELE CHA TUZO YA MWALIMU NYERERE YA UANDISHI BUNIFU ,APRIL 13 2023 KUFANYIKA DAR

    March 30, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.