Site icon A24TV News

NCHI ZINAZOZALISHA ALMASI BARANI AFRIKA(ADPA )ZAKUBALIANA KUFANYA MAREKEBISHO YA KATIBA YA UMOJA HUO.

 

Na .Mwandishi wanA24Tv Arusha

Umoja wa nchi zinazozalisha almasi barani Afrika (ADPA) zimekubaliana kupitia upya na kurekebisha katiba na miongozo ya umoja huo kwa kuwa ile ya awali inepitwa na wakati.

Hayo yamesemwa leo na waziri wa madini nchini,Dotto Biteko katika mkutano wa ADPA unaondelea jijini Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari Waziri Biteko alisema kwamba tayari timu ya wataalamu imeshakamilisha nyaraka ambapo wataziwasilisha kwenye baraza la mawaziri ili ziweze kupitiwa .

Waziri Biteko alisema kwamba wamejiridhisha kwamba nyaraka hizo zinahitaji marekebisho ili ziweze kuendana na wakati.

“Leo zege halilali tunataka kuhakikisha tunakamilisha nyaraka za kuongoza ADPA ili kupitisha katiba iendane na wakati “alisema Biteko

Waziri Biteko alisisitiza kwamba umoja huo leo unataraji kukamilisha kazi ya kuajiri watendaji kwa kuwa waliokuwepo wametoa nchini Angola na wanafanya kazi kama hisani.

“Kazi tuliyonayo leo pia tuna agenda ya kuajiri watendaji kwani waliokuwepo wanatokea Angola na wanafanya kazi kama hisani hatuwezi kuwa na umoja wenye nguvu wakati una watendaji wa kuazima “alisisitiza Waziri Biteko

Hatahivyo,waziri Biteko alisisitiza kwamba mbali na umoja huo kuwa na wanachama 19 tayari kuna nchi 6 barani Afrika zimeomba kujiunga na mchakato bado unaendelea.

Mwisho.