Site icon A24TV News

RAIS DK. MWINYI APOKEA SALAMU ZA POLE KUTOKA KWA MH.MASAUNI

Na Mosses Mashala Zanzibar.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amepokea salamu za pole nyumbani kwake Ikulu Migombani kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Hamad Yussuf Masauni kufuatia kifo cha Baba Mzazi, Rais Mstaafu wa Zanzibar na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Mzee Ali Hassani Mwinyi aliyefariki dunia tarehe: 29 Februari 2024, Dar es Salaam na kuzikwa tarehe: 02 Machi 2024, Mangapwani, Mkoa wa Kaskazini, Unguja.

Mwisho .