Site icon A24TV News

MADARASA YA KISASA YA SHILINGI MILION 42 YA SHULE YA SEKONDARI KILIMAJI KUTOKA BANK YA CRDB YAKABIDHIWA SERIKALI

Na Geofrey Stephen Arusha.

BENKI ya CRDB imeikabidhi Wilaya ya  Arusha Madarasa ya kisasa mawili vyenye thamani ya sh,milioni 42 katika shule ya Sekondari Kilimaji ya Jijini Arusha hiliyopo katika kata ya Moshono yakabidhiwa katika Mkoa wa Arusha  ikiwa ni jitihada za kuunga mkono serikali katika kuboresha miundo ya elimu Nchini.

 

Akiongea katika hafla hiyo ikiwa ni sehemu ya kuelekea mkutano mkuu wa 28 wa wanahisa wa CRDB, iliyofanyika katika shule hiyo, iliyopo kata ya Moshono,jijini Arusha.

Mkurugenzi mtendaji wa benki  ya CRDB, Abdulmajid Nsekela alisema msaada huo umetokana na sera ya benki hiyo kurudisha asilimia moja ya mapato yake kwa jamii.

“Benki yetu imekuwa ikitenga asilimia moja ya pato lake ili iweze kujeresha kwa jamii katika maeneo makuu ya elimu,Afya  na mazingira pamoja na kuwezesha makundi maalumu ya akina mama na vijana”

Katika muktadha huo benki ilipokea maombi ya uhitaji wa madarasa hayo katika shule hiyo ya sekondari Kalimaji iliyoanzishwa januari 2022  ikiwa na wanafunzi 58.

Mkurugenzi huyo alisema kwakuwa maombi hayo yanayoendana na  sera ya uwekezaji kwa jamii katika nyanja ya elimu,benki hiyo iliridhia ombi hilo  na kutoa kiasi cha sh,milioni 42 kujenga madarasa hayo.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi huyo alipokea ombi la Uhitaji wa jengo la maabara pamoja na vishkwambi kwa wanafunzi na kutoa mchango wa sh,milioni 10 kwa ajili ya maombi hayo.

Alitoa rai kwa uongozi wa shule hiyo kutunza majengo hayo ili yasaidie vizazi vijavyo ,pia aliwaomba wazazi kuwafungulia akaunti watoto wao ili kuiwezesha benki hiyo kujiendesha na kuendelea kuisaidia jamii.

Naye mkuu wa wilaya ya Arusha ,Felisian Mtehengerwa aliishukuru  benki ya CRDB kwa msaada huo wa kizalendo na kueleza namna utakavyoweza kusaidia kupunguza changamoto ya msongamano kwa wanafunzi .

Hata hivyo alisisitiza kuwa serikali ya awamu ya sita imewekeza zaidi katika sera ya elimu hasa ujenzi wa miundo mbinu ya madarasa na kuifanya elimu ya sekondari kuwa bure.

“Benki ya CRDB kukabidhi haya madarasa mawili ni ishara kwamba benki hiyo imeonyesha uzalendo mkubwa kwa kuunga mkono jitihada za rais Samia suluhu Hasan katika sekta ya elimu “

Awali mbunge wa Arusha mjini Mrisho Gambo alitoa rai kwa wananchi kuweka uzalendo mbele kwa kuitumia benki CRDB kufungua akaunti ili kuinua uchumi wa taifa kwani benki hiyo imekuwa mahususi kurejesha sehemu ya faida kwa jamii.

Aliiomba benki hiyo kuona umuhimu wa kuendelea kuisaidia shule hiyo ambayo bado inachangamoto kubwa ikiwemo ujenzi wa jengo la utawala pamoja na uhitaji wa kompyuta kwa wanafunzi.

.
Hata hiyo  mkuu huyo wa wilaya alimhakikishia mbunge huyo kwamba suala ya Kompyuta atalitatua kupitia wadau wa maendeleo na kuitaka benki hiyo kujikita zaidi kusaidia ujenzi wa jengo la maabara.
Miongoni mwa viongozi mashuhuri waliohudhulia hafla hiyo ni pamoja na Mkurugenzi wa CRDB nchini Burundi, Fredrick Siwale,Meya wa jiji la Arusha, Maximilian Iranghe, Mkurugenzi wa jiji la Arusha Hargeney Chitukuro pamoja na viongozi mbalimbali wa eneo hilo.
Ends..