Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»WAKALA WA MISITU WAPANGA KUKUSANYA BILION 3.7

    WAKALA WA MISITU WAPANGA KUKUSANYA BILION 3.7

    0
    By arushatv on November 1, 2022 Habari
    Na Geofrey Stephen Lushoto .

    WAKALA wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), kupitia shamba la Miti la  Shume,lililopo Wilayani Lushoto, Mkoa wa Tanga katika mwaka wa fedha 2022/23 imepanga kukusanya mapato ya serikali ya shilingi Bilioni 3.7.

    Makusanyo hayo yanatokana na mauzo ya mazao ya miti na zao la nyuki  .
    Akiongea na waandishi wa habari waliotembelea shamba hilo katika ziara ya Mkuu wa wilaya ya Lushoto,Kalisti Lazaro,Mhifadhi Mwandamizi wa Shamba hilo,Ernest Madata alisema mwaka wa fedha 2020/21 walishindwa kufikia malengo ya kukusanya sh,bilioni 3.8 waliojiwekea na kukusanya sh,bilioni 2.2 sawa na asilimia 59.4.
    Alisema kutofika kwa malengo hayo  kulichangiwa na changamoto  mbalimbali ikiwemo kushuka kwa zao la mbao na Nyuki kulikochangiwa na janga la UVIKO-19.
    Mhifadhi huyo alisema kuwa changamoto hiyo ilipelekea kushuka pia kwa  malengo ya makusanyo ya halimashauri ya sh,miliojin108 na kufanikiwa  kukusanya sh,milioni 74.5 tu sawa na asilimia 68.49.
    Alisema mwaka huu wa fedha 2022/23 wamepanga kuvuka lengo la makusanyo kwani hadi hivi sasa wameshafikia asilimia 16 ya makusanyo jambo ambalo alidai watavuka malengo waliojiwekea.
    Madata alisema Shamba la Shume ni moja kati ya mashamba makubwa ya miti yanayomilikiwa na TFS lenye ukubwa wa ekari 4863 ambalo lilianzishwa mwaka 1926 kwa lengo la kuendeleza shughuli za upandaji miti kwa ajili ya utunzaji wa mazingira na ukusanyaji wa maduhuli ya serikali.
    Pia alisema faida ya shamba hilo ni pamoja na kutoa kwa ajira kwa wananchi wilayani humo ambapo kwa mwaka  wananchi wapatao 200,000 wananufaika na ajira na hivyo kujiongezea kipato.
    ‘Uwepo wa shamba la miti wilayani Lushoto katika kipindi cha mwaka wa fedha uliopita 2020/2021 wamechangia sh,milioni 260 kuboresha miundombinu ya barabara yenye urefu wa kilometa 14.4 iliyopo katika jamii inayowazunguka “
    Awali mkuu wa wilaya Lushoto, Kalisti Lazaro aliipongeza TFS kwa kuchangia maendeleo wilayani huo na kuitaka kuongeza jitihada zaidi ili kufikia malengo waliyojiwekea .
    Lazaro alisema kuwa TFS kupitia shamba hilo imechangia kupunguza suala la ajira wilayani humo hususani vijiji vinavyozunguka shamba hilo na kuwataka wananchi kulitumia shamba hilo kuongeza vipato vyao na kukuza uchumi wa taifa.
    Ends…
    Post Views: 85
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleDC IKUNGI AWAPELEKA WATATU TAKUKURU KUKWAMISHA UJENZI KITUO CHA AFYA IRISYA.WAMALIZA MILIONI 500
    Next Article MONGELA AVUTIWA NA JENGO LA HOSPITAL CHUO CHA ATC LA BILION 1.384

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.