Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»TAASISI NA WATENDAJI WA TAASISI ZA UMMA WAHAKIKISHE MAZINGIRA WEZESHI YA BIASHARA NA UWEKEZAJI.

    TAASISI NA WATENDAJI WA TAASISI ZA UMMA WAHAKIKISHE MAZINGIRA WEZESHI YA BIASHARA NA UWEKEZAJI.

    0
    By arushatv on November 2, 2022 Habari

    Na Mwandishi wa A24Tv .

    Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara – Viwanda na Biashara Dkt. Hashil Abdallah amezishauri Taasisi za umma pamoja na watendaji wake wanaotoa huduma kuhakikisha wanaweka mazingira bora ya biashara na uwekezaji ili kifikia malengo ya Serikali ya Awamu ya Sita na kuliwezesha Taifa kufikia uchumi wa Kati wa Juu.

    Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara Dkt. Abdallah katika ufunguzi wa semina ya Wajumbe wa Baraza la Ushindani iliyofanyika Novemba mosi (1) 2022 katika ukumbi wa Chuo cha Uvuvi, Mbegani, Bagamoyo amesema mazingira bora na wezeshi ni muhimu katika kuvutia wawekezaji, kuendeleza viwanda na kufanya biashara nchini.

    Dkt. Abdallah pia amewashauri Wajumbe wa Baraza hilo kuainisha Sheria, Kanuni na Taratibu zote zinazosimamia sekta ya uwekezaji na biashara zenye changamoto katika uwekaji wa mazingira wezeshi ya biashara na uwekwzaji nchini ili zifanyiwe maboresho ziwezw kuendana na mabadiliko ya ukuaji wa uchumi na zikidhi mahitaji.

    Naye Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani (FCT) Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu-Divisheni ya Kazi, Mhe. Salma Maghimbi amesema Baraza hilo litaendelea kutenda haki katika maamuzi yake kwa kuzingatia sheria, kanuni taratibu pamoja na ushahidi na udhibiti unaotolewa kwa lengo la kuendeleza biashara, kuvutia uwekezaji na hatimae kukuza uchumi wa Taifa.

    Naye Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC) Bw. William Erio amesema FCC inashirikiana na FCT katika kuliwezesha Baraza kufanya maamuzi ya kesi zinazowasilishwa kwa Baraza hilo kutoka Mamlaka za Udhibiti mbalimbali ili kuhakikisha biashara zinaendelea kwa kizingatia usawa katika ushindani wa soko.

    Akitoa taarifa ya utendaji kazi mbele ya Mgeni Rasmi, Msajili wa FCT, Mhe. Renatus Rutatinisibwa amesema Baraza hilo linajukumu la kupokea, kusikiliza na kutolea maamuzi kesi mashauri ya rufaa yatokanayo na ushindani wa kibiashara na udhibiti wa soko kutoka FCC, EWURA, LATRA, TCAA, TCRA na PURA.

    Aidha, amesema Baraza hilo limepewa hadhi ya Kimahakama ya utoaji haki kwenye masuala ya Ushindani Udhibiti wa Soko naKumlinda mlaji. Maamuzi ya kesi za rufaa na maombi yanayotolewa na Baraza hilo ni ya mwisho.

    Post Views: 66
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleCHADEMA YANUSA UFISADI MIRADI YA NSSF ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV
    Next Article Mzuka Nusu Fainali Chemchem CUP 2022 kuanza leo kuwania mamilion Babati.

    Related Posts

    Kamati yapitisha makadirio ya matumizi na maendeleo 2023/2024 kwa Wizara Uwekezaji Viwanda na Biashara.

    March 23, 2023

    MWANDISHI WA HABARI MAARUFU ALLAN ISACK AITAKA NAFASI YA MNEC

    March 23, 2023

    Vyombo vya Dola na wanasheria kushirikiana kutokomeza ujangili Babati

    March 22, 2023

    JIJI LA ARUSHA LATOA MIKOPO YA SHILINGI BILION 2.6 KWA VIJANA WENYE MAITAJI MAALUM NA WANAWEKE

    March 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.