Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Health»MONGELA AVUTIWA NA JENGO LA HOSPITAL CHUO CHA ATC LA BILION 1.384

    MONGELA AVUTIWA NA JENGO LA HOSPITAL CHUO CHA ATC LA BILION 1.384

    0
    By arushatv on November 1, 2022 Health
    Mkuu wa mkoa wa Arusha,John Mongella amekitaka chuo cha ufundi Arusha ATC,kuhakikisha huduma zitakazotolewa katika  mradi wa hospitali unaojengwa chuoni hapo,unaimarisha sekta ya afya  nchini  na kukidhi mahitaji ya afya kwa wanafunzi  , jamii na  watalii.
    Akiongea mara baada ya kuweka jiwe la msingi katika mradi huo wa jengo la hospitali ya kufundishia na Tiba ( Polyclinic )katika chuo hicho ,alisema Kliniki hiyo ikikamilika isaidie kutoa huduma za kiwango cha juu kwa wanafunzi kujifunzia na tiba kwa wananchi.
    Alisema kuwa ubora wa huduma zitakazotolewa katika hospitali hiyo uwe wa kiwango cha juu na uendane na hadhi ya majengo na kukidhi huduma za afya kwa watalii .
    “Niwapongeze sana kwa matumizi sahihi ya fedha za mradi nipo tayari hata kumleta rais Samia Suluhu kufungua jengo hili ninachowaomba mjitanzaze na sisi kama mkoa tutaendelea kuwatangaza”
    Katika hatua ngingine Mongela alikipongeza chuo hicho kwa kutekeleza mradi huo kwa ubora na gharama nafuu ya sh,bilioni 1.384  na kuahidi miradi mingine ya serikali mkoani hapo kukipatia chuo hicho   kwani kimeonesha uzalendo na nidhamu ya matumizi ya fedha za umma.
    Awali mkuu wa chuo hicho,Mussa Chacha alisema hospitali hiyo imetekelezwa na chuo hicho kupitia mapato yake ya ndani ,ambapo kiasi cha sh,bilioni 1,384,301,300 kilitengwa.
    Alisema  hospitali  hiyo itatatua upungufu wa miundombinu ya kufundishia mafunzo  kwa vitendo ,tafiti nanhudumanbora za matibabu kwa wananchi wa jiji la Arusha.
    Alisema kwa sasa hospitali hiyo imefikia asilimia 92,na kiasi cha sh,bilioni 1.064 kimetumika hadi sasa na ujenzi huo unatarjiwa kukamilika mwishoni mwa mwezi Novemba, mwaka huu 2022 .
    Alisema hospital  hiyo inakadiliwa  kutoa huduma kati ya  watu 100 hadi 300 kwa siku ikihudumia wanafunzi,wafanyakazi na wananchi  katika huduma za uchunguzi wa afya ,huduma ya mama na mtoto , huduma  ya macho,mfumo wa pua ,koo ,masikio ,meno magonjwa ya ndani ,huduma za upasuaji ,utoaji dawa na vifaa tiba.
    Ends..
    Post Views: 170
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleWAKALA WA MISITU WAPANGA KUKUSANYA BILION 3.7
    Next Article CHADEMA YANUSA UFISADI MIRADI YA NSSF ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV

    Related Posts

    MIAKA 5, YA MREMBO MASIPETII MSICHANA MDOGO ALIYEJITOLEA KUSAIDIA JAMII NA KUACHA KAZI, ANAMILIKI NYUMBA YA MILLION 280

    March 11, 2023

    DKT MOLLEL ATOA MAJIBU MALALAMIKO UBOVU WA CHF.

    February 23, 2023

    APOTEZA MAISHA KWA KUCHAPWA FIMBO 70 ZA KIMASAI ! KOSA LA KUMTUKANA MAMA YAKE MZAZI MATUSI YA NGUONI

    January 10, 2023

    DC RUNYANGO VIJANA MJITAMBUE KATIKA AFYA NDIO MAISHA ,MJIKINGE NA MAAMBUKIZI

    December 12, 2022

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.