Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»FRANK BATEZI NA NICO NGOWO MBARONI KWA KUBAKA, KULAWITI NA KUMUINGIZIA CHUPA MUUZA BAA

    FRANK BATEZI NA NICO NGOWO MBARONI KWA KUBAKA, KULAWITI NA KUMUINGIZIA CHUPA MUUZA BAA

    0
    By arushatv on November 21, 2022 Habari

     

    Na Mwandishi wetu, Mirerani

    Wakazi wawili wa mji mdogo wa Mirerani Wilayani Simanjiro Mkoani Manyara, Frank Msuya Batezi na Nico Anthony Ngowo, wanashikiliwa na polisi kwa kumbaka msichana muuzaji wa baa na kisha kumuingizia chupa ya bia njia ya haja kubwa.

    Batezi na Nico inadaiwa kuwa walishirikiana na wenzao wengine wawili ambao walikimbia, kumbaka na kumlawiti msichana huyo kisha kumuingizia chupa ya bia njia ya haja kubwa.

    Kamanda wa polisi wa mkoa wa Manyara, George Mutabazi amethibitisha kukamatwa kwa watu wawili kwa kudaiwa kumbaka na kumlawiti msichana huyo.

    Kamanda Mutabazi amesema wanatarajia kuwafikisha mahakamani watuhumiwa hao wawili wakati wowote ili wakajibu mashtaka hayo yanayowakabili kwani uchunguzi umekamilika.

    Mmoja kati ya shuhuda wa tukio hilo, Hassan Juma amesema Batezi na Nico walikuwa wanakunywa pombe na msichana huyo eneo la Songambele kasha wakaenda Kazamoyo kulala.

    Amesema walishirikiana watu wanne kumfanyia kitendo hicho cha kikatili kwa kumbaka, kumlawiti kisha kumuingizia chupa ya bia kwenye sehemu ya haja kubwa.

    “Ni kitendo cha kinyama mno walichokifanya Batezi na huyu Nico ambaye ni raia wa Kenya kwani dada wa watu aliharisha na damu kuvuja kwenye njia ya haja kubwa,” amesema.

    Mganga wa mfawidhi wa kituo cha afya Mirerani Dk Deogratius Mazengo amethibitisha kutibiwa hapo kwa msichana huyo ambaye alifika na fomu namba tatu ya polisi.

    MWISHO

    Post Views: 119
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMTIKISIKO BIASHARA YA KUKU NCHINI ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV
    Next Article CHAGUZI ZAFUTWA RUSHWA NJE NJE ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.