Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»WIZARA YA HABARI TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YAWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYUO MASWALA YA MTANDAO

    WIZARA YA HABARI TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YAWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYUO MASWALA YA MTANDAO

    0
    By arushatv on October 17, 2022 Habari
    Na Geofrey Stephen Arusha.

    WIZARA ya Habari Teknolojia ya Habari na Mawasiliano imewataka wananchi kutambua kuwa suala la uchunguzi wa simu zilizopotea katika
    jeshi la Polisi nchini ni huduma ya Bure ambayo haina malipo yeyote.

    Akizungumza na Uongozi na wanafunzi wa Vyuo vya Uhasibu IIA na Ufundi ATC jijini Arusha Mtaalamu wa Usalama wa mtandao na uchunguzi wa
    makosa ya Kidigitali Yusuph Kileo amesema kwamba ipo haja kwa wananchi kujengewa uelewa wa matumizi salama ya makosa na uhalifu wa mtandao.

    Kwa mujibu wa Mtaalamu huyo Uelewa huo utsaidia sana jamii kuelimishwa kuhusu sheria kanuni na miongozi inayosimamia usalama Mtandao hapa nchini wkati huu wa mageuzi ya kiuchumi kwa njia ya kidigiti.

    Alisema kwamba wapo wengi ambao Nyilawila zao wamekuwa hawaziweki katika usalama na kupelekea wahalifu kutumia kurasa zao za mitandao ya
    kijamii kiuhalifu hivyo busara kwao ni kuweza kujengewa uelewa utakaosaidia kuepuka na kuwa salama

    “Hivi sasa serikali inaendelea kutoa elimu kwa wadau wake ndani ya serikali ambao utasaidia kuondoa uhalifu wa kuingia kwenye mifumo bila kuingiza nyilawila ya ofisa muhusika hivyo kama watu hawapati uelewa
    na elimu kutakuwa na mianya ya uhalifu.

    Kwa Uapnde wake   Mkuu wa Chuo cha Ufundi Arusha Musa Mhandisi Chacha amesema mafunzo hayo ya usalama kwa njia ya mtandao yatasaidia
    kuongeza uelewa wa matumizi sahihi ya mitandao nchini na kuondokana na
    uhalifu wa kimtandao.

    Akatoa wito kwa Wizara kwanda kwa wananchi wakati huu uchumi ukielekea katika mitandao kutuma na kuagiza sanjari na malipo kwa njia hiyo
    hivyo uelewa ukiwafikia wananchi utasaidia sana kuondoa changamoto wanazokumbana nazo.

    Awali akiongea Mkurugenzi wa Mawasiliano kutoka wizara ya Habari teknolojia ya Habari na mawasiliano amesema kwamba tokea mwaka 2018 kazi ya kuangalia usalama mtandao nchini na maboresho yake umeendelea kufanyika na serikali.

    Alisema kwamba ipo misingi mitano mikuu ya uboreshaji ambyo ni miundombinu wezeshi Teknolojia wezeshi Sheria wezeshi Utaalamu sanjari na mazingira ya udhibiti wao kwa sasa wapo katika kampeni ya kutoa
    elimu na kuutambulisha mfumo huo wakati akijipanga kuwaendea wananchi.

    Mwisho
    Post Views: 88
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleWaziri Ndumbaro WANANCHI WABORESHEWA MFUMO WA TEHAMA KATIKA UTOAJI HAKI NCHINI
    Next Article ASKOFU ALIA NA NDOA JINSIA MOJA NI ATARI KULIKO CORONA ! MAGAZETI YA LEO ARUSHA 24TV

    Related Posts

    SERIKALI YAFUNGIA MGODI WA GEM AND ROCK VENTURE ULIOKO MIRERANI

    March 20, 2023

    TRA CHUNYA KUSAMBAZA ELIMU YA MLIPA KODI KWA WACHIMBAJI WA DHAHABU.

    March 16, 2023

    Wizara ya Madini imefanikiwa kutaifisha madini ya Tanzanite yenye uzito wa kilo 4 yenye thamani ya mamilioni ya fedha  kutoka kwa Meneja wa Mgodi wa Gem & Rock Venture

    March 16, 2023

    DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

    March 16, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.