Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»Waziri Ndumbaro WANANCHI WABORESHEWA MFUMO WA TEHAMA KATIKA UTOAJI HAKI NCHINI

    Waziri Ndumbaro WANANCHI WABORESHEWA MFUMO WA TEHAMA KATIKA UTOAJI HAKI NCHINI

    0
    By arushatv on October 17, 2022 Habari

    Na Geofrey Stephen Arusha

    Wizara ya Katiba na Sheria Imeeleza kwamba imejipanga katika mfumo wa
    Tehama katika utoaji haki nchini utaosaidia kuboresha kurahisisha na
    kuondoa changamoto za wananchi kufuata huduma umbali mrefu.

    Aidha Serikali imeweka mazingira mazuri ya mfumo wa kidigiti kuweza
    kupatikana katika Katiba na sheria sanjari na elimu mtandao ya sheria
    ili wananchi waweze kupata huduma hizo kwa urahisi Popoto walipo.

    Hayo yamesemwa na Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro
    wakati akizindua mafunzo ya mifumo ya Tehama kwa sekta ya sheria kwa
    wadau wa huduma za kisheria kwa siku mbili jijini Arusha.Alisema kwamba katika Bajeti ya mwaka huu waliweka vipaumbele 14
    ikiwemo matumizi ya Tehama katika mifumo ya utoaji haki nchini na
    kuanisha kuwa wameafanikiwa katika mhimili wa mahakama.

    Kwa Mujibu wa Waziri Ndumbaro amesema kama wizara wanajukumu kubwa
    katika utoaji wa elimi juu ya katiba na sheria kupitia Tehama pamoja
    na kuweka mahakama ya mwanzo kila tarafa kurahisisha utoaji haki kwa
    wananchi.Kwa upande wake mkuu wa kitengo cha tehama wizara ya katiba na sheria
    Gabriel Omari amesema lengo kubwa la mafunzo haya ni kuhakikisha wadau
    wa sheria wanaweza Kutumia mfumo wa tehama kujisajili popote walipo
    badala la kwenda wizarani sanjari na shughuli zote za wizara kufanyika
    kwa njia ya Mtandao.

    Alisema lengo la Mafunzo hayo ni kutoa uelewa mpana kwa washiriki hao
    katika Tehama kwa kwa kuwa tokea kuanzishwa kwa mfumo huo kumekuwa na
    changamoto ya uelewa hivyo kuchelewesha wananchi kupata huduma.Awali Msajili wa watoa huduma za msaada wa kisheria Nchini Felista
    Mushi amesema Mafunzo hayo yamewashirikisha watoa huduma za kisheria
    kutoka mikoa 10 wasajili wasaidizi  pia kutoka mikoa kumi pamoja na
    maafisa Magereza na Polisi waliopata mafunzo ya msaada wa kisheria.

    Alisema kwamba washiriki hao wamechaguliwa kwa sababi wapo karibu na
    wananchi sanjari na kuwasaidia wananchi wengi wa chini waliopo maeneo
    mbalimbali nchin lengo ni wizara kuingia katika mfumo wa utoaji haki
    hususani haki jinai kwa urahisi.
    Post Views: 97
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleRAIS SAMIA BITEKO ANATOSHA WIZARA YA MADINI ! MAGAZETI YA LEO ARUSHA 24TV
    Next Article WIZARA YA HABARI TEKNOLOJIA NA MAWASILIANO YAWAPIGA MSASA VIONGOZI WA VYUO MASWALA YA MTANDAO

    Related Posts

    Tanzania na India kuendeleza Uhusiano wa Kibiashara na Uwekezaji

    March 27, 2023

    TANZANIA YAKABILIWA NA UHABA WA MABAHARIA VIJANA.

    March 27, 2023

    Marcas Ajitosa kuwania U NEC Arusha

    March 25, 2023

    VIKUNDI 47 KUPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOITA MONDULI

    March 24, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.