Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Elimu»Wanafunzi wa kike waliokosa Masomo ya Sekondari wapata ufadhili

    Wanafunzi wa kike waliokosa Masomo ya Sekondari wapata ufadhili

    0
    By arushatv on October 25, 2022 Elimu

    Na Doreen Aloyce, Dodoma

    Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima Dkt.Emanuel Ng’umbi amesema kuwa Taasisi imefanikiwa kuwafikia wasichana 3,333 sawa na asilimia 111 ya lengo ambao walishindwa kuendela na shule ya sekondari kutokana na mazingira magumu, kupata ujauzito na ndoa za utotoni.

     

    Dkt. Ng’umbi ambapo ameyabainisha leo Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa wameendesha mafunzo kwa nyakati tofauti kwa wasimamizi na watendaji, wawezeshaji na walimu wa madarasa ya mradi wa SEQUIP.

    “Kwa mwaka 2022/2023, TEWW itaendelea kushirikiana na Wizara ya Elimu Sayansi na Tekonolojia katika kuandaa Juma la Elimu ya Watu Wazima kwa mwaka 2023,Vile vile, TEWW itahamasisha, kusajili na kufundisha wanafunzi 3,000 wa mradi wa SEQUIP kwa mwaka 2023,”amesema.

    Amesema kuwa TEWW inatarajia kupanua mpango wa IPOSA katika mikoa mipya sita (6), kwa kujenga karakana za kufundishia, na pia kupanua mafunzo ya TEHAMA kwa wanafunzi wa IPOSA,Kwa upande wa programu ya IPPE, TEWW inatarajia kuanza kusajili vituo vya mafunzo vitakavyotumia mtaala ulioboreshwa wa IPPE.

    Ameeleza kuwa TEWW imekusanya takwimu za hali ya kisomo kutoka mikoa yote ya Tanzania bara na inaendelea na uchambuzi wa taarifa na takwimu hizo ikiwa ni hatua ya mwanzo ya utafiti wa hali ya kisomo na elimu kwa umma nchini.

    “Katika mwaka 2022/2023 TEWW itaendelea kutekeleza majukumu yake katika eneo hili, ikiwa ni pamoja na kuendelea kuwatumia wanachuo wake katika kufungua vituo vya kisomo nchi nzima ikiwa ni sehemu ya mafunzo kwa vitendo, TEWW pia inatarajia kuandaa, kuchapisha na kusambaza ripoti ya hali ya kisomo katika mikoa ya Tanzania bara,

    Kuboresha miundombinu ya ujifunzaji na ufundishaji Katika mwaka 2021/2022, kwa kupitia mradi wa SEQUIP, TEWW ilikarabati majengo ya ofisi na madarasa katika mikoa minne ya Dar es Salaam, Morogoro, Ruvuma, na Dodoma. Halikadhalika, TEWW ilianza ujenzi wa majengo ya ofisi na madarasa katika mikoa minne ya Pwani, Rukwa, Iringa na Manyara,”amesema.

    Aidha amesema kuwa Jumla ya TZS bilioni 1,200,000,000) kimetumika,Pia TEWW ilianza ujenzi wa jengo la utawala katika kampasi ya Morogoro kwa kutumia fedha kutoka serikali kuu.

    Amesema Kiasi cha TZS 500,000,00 kilitolewa na serikali kuu kwa ajili ya kazi hiyo kwa mwaka 2021/2022,Katika mwaka wa 2022/2023, TEWW inatarajia kuendelea na ujenzi wa madarasa na ofisi katika vituo vya mikoa sita (6) na ukarabati katika vituo vya mikoa miwili.

    Ikumbukwe kuwa Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima (TEWW) ni Taasisi ya Umma iliyoanzishwa chini kwa Sheria ya Bunge Na. 12 ya Mwaka 1975; ikiwa ni taasisi chini ya Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambayo jukumu la TEWW kusimamia elimu ya watu wazima na elimu nje ya mfumo rasmi nchini.

    • Mwisho..
    Post Views: 73
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleIGP ,KULA SAANI MOJA POLISI WALIO SABABISHA MAUAJI, MOROGORO ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV.
    Next Article WALIMU WAFUTWA KAZI ,SHULE YAFUNGIWA ! KISA NAMBA YA MTIHANI ,MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV

    Related Posts

    SHULE YA BILIONEA SANINIU LAIZER YAPATA UFADHILI MZITO WA MADAWATI NA MEZA ZA KISASA

    March 13, 2023

    Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Carolyne Nombo amewataka watumishi wa Wizara hiyo kufanya kazi kwa umahiri.mkubwa

    February 28, 2023

    WIZARA YA ELIMU YATOA UFAFANUZI WALIO FUTIWA MATOKEO YA MITHIANI WA KIDATO CHA NNE

    February 9, 2023

    WANAFUNZI 170 WAPATIWA MSAADA WA VIFAA VYA SHULE KUTOKA OFISI YA MBUNGE WA JIMBO LA MONDULI.

    January 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.