Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Break News»DC LUSHOTO KALIST, AMVAA VIKALI MKANDARASI! ALIYEKWAMISHA MRADI WA MAJI WA BILIONI 1.8

    DC LUSHOTO KALIST, AMVAA VIKALI MKANDARASI! ALIYEKWAMISHA MRADI WA MAJI WA BILIONI 1.8

    0
    By arushatv on October 26, 2022 Break News, Habari
    Na Geofrey Stephen ,Lushoto
    Mkuu wa Wilaya ya Lushoto Mkoani Tanga,Kalist Lazaro amewataka Wakurugenzi wa Kampuni ya M/S PNR SERVICES ya Jijini Dar es Salaam waliopewa zabuni ya shilingi Bilioni 1.8 ya kuvuta maji km 14 kutoka
    Hifadhi ya Msitu wa Magamba hadi katika Mji wa Lushoto kujisamilisha wenyewe ofisini kwake kwa nini hadi Sasa wameifanya kazi hiyo kwa asilimia 20 tu.

    wakati mradi huo wanapaswa kuukabidhi kwa Mamlaka ya maji Lushoto(RUWASA) januari 30 mwaka kesho.

    Lazaro alisema hayo katika chanzo Cha maji Cha Msitu huo alipotembelea Mradi huo na kusikitishwa kuona Mkandarasi amelipwa zaidi ya shilingi milioni 200 kwa ajili ya kazi hiyo lakini amekuta wafanyakazi saba tu

    katika ujenzi wa chanzo Cha maji Hali iliyomsikitisha na kupata taarifa kuwa Wakurugenzi wa Kampuni hawajawahi fika Lushoto pamoja na kutakiwa na uongozi wa RUWASA zaidi ya Mara tatu.
    Mradi wa ujenzi wa maji ukionekana katika ujenzi kwa asilimia% 20 
    Alisema na kumwagiza msimamizi wa mradi wa Kampuni hiyo, Singo Omari aliyemkuta eneo la Mradi kuwataarifa Wakurugenzi wake kuwa anawahitaji
    haraka ofisni kwake Alhamis  octoba 27 mwaka huu saa 1.30 asubuhi kufika bila kukosa  kujieleza Ni kwa Nini wasichukuliwe hatua kwa kupuuza wito wa Meneja

    wa RUWASA Wilaya ya Lushoto na kwa nini kazi haifanyiki wakati wameshachukua mamilioni ya pesa za Serikali kwa ajili ya Mradi huo.

    Mkuu wa Wilaya alisema tanki ya maji lenye uwezo wa kubeba Lita 600,000 bado halijajengwa,usambazaji wa bomba za maji za umbali wa km 14 kutoka Msitu wa Magamba hadi Mjini Lushoto bado mtaro haujachimbwa Wala mabomba hayajafika eneo la Mradi na alisema dharau za Wakurugenzi wa Kampuni ya M/S PNR SERVICES waliifanya haitavumiliwa kamwe lazima
    waeleze ni kwa nini muda wote hawajafanya kazi na pesa ya Serikali wameshapewa.

    ” Waambie Wakurugenzi wako nawahitaji ofisini kwangu Alhamis asubuhi
    saa 1.30 hii haikubaliki na sitakubali Wilaya niliyokabidhiwa na Rais
    Mkandarasi afanye anavyotaka katika Miradi ya Maendeleo  hii
    haikubaliki hatua lazima zichukuliwe ” alisema Lazaro

    Naye Meneja wa RUWASA katika Wilaya ya Lushoto, Erwin Sizinga alisema kuwa Mkurugenzi wa Kampuni hiyo hawana ushirikiano na ofisni yake kwani wamekuwa wakifanya kazi wanavyotaka na kutoa sababu nyingi zisizokuwa na Msingi toka walipopewa kazi hiyo March Mwaka huu pamoja
    na kupewa kiasi Cha zaidi ya shilingi milioni 200 walizoomba katika malipo ya awali.

    Meneja wa Ruwasa akizungumza na waandishi wa habari ya juu ya mradi huo kusua sua 

    Sizinga alisema mahitaji ya maji katika wilaya ya Lushoto ni lita milioni 12.3 kwa siku na kwa sasa lita milioni 8.3 kwa siku maji yanatoka na kuna upungufu wa maji lita milioni 3.9 kwa siku na iwapo miradi yote itakamilika kuna uwezekano mkubwa wa kupatikana kwa maji kwa wingi katika wilaya hiyo.

    Alisema Mji wa Lushoto una hitaji Sana maji kutoka chanzo Cha Msitu wa Asili wa Magamba na Mradi huo ukikamilika una uwezo wa kutoa Lita 150,000 hadi 160,000 kwa saa kutoka katika chanzo hicho na Mradi huo ukikamilika huenda shida ya maji katika Mji wa Lushoto na wenye kata 51 na vijiji 208 ukaisha.

    Alisema Changamoto ya maji katika wilaya ya Lushoto kwa Sasa ni asilimia 68 na iwapo Miradi yote ya maji ikikamilika Changamoto hizo zitakwisha na maji yatakuwa mengi katika Wilaya hiyo yenye biashara
    kubwa ya matunda na mboga mboga.

    Naye Meneja wa Kampuni ya M/S  PNR SERVICES ,Omari Singo alikiri kutokamilkika ndani ya muda kwa mradi huo na kumwomba Mkuu wa Wilaya kumpa muda zaidi ili aweze kuzungumza na Wakurugenzi wa Kmapuni hiyo ili waweze kumpa ,ajibu sahihi juu ya mradi ili unaweza kukamilika.

    Mwisho

    Post Views: 115
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleWALIMU WAFUTWA KAZI ,SHULE YAFUNGIWA ! KISA NAMBA YA MTIHANI ,MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV
    Next Article RAIS SAMIA AWEKA HISTORIA UJENZI WA HOSPITALI YA MAMA NA MTOTO LUSHOTO DC TUMESIMAMIA ILANI

    Related Posts

    Kamati yapitisha makadirio ya matumizi na maendeleo 2023/2024 kwa Wizara Uwekezaji Viwanda na Biashara.

    March 23, 2023

    MWANDISHI WA HABARI MAARUFU ALLAN ISACK AITAKA NAFASI YA MNEC

    March 23, 2023

    Vyombo vya Dola na wanasheria kushirikiana kutokomeza ujangili Babati

    March 22, 2023

    JIJI LA ARUSHA LATOA MIKOPO YA SHILINGI BILION 2.6 KWA VIJANA WENYE MAITAJI MAALUM NA WANAWEKE

    March 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.