Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Makala»POLISI NJOMBE WAKIRI KUNA SHIDA YA MIGOGORO

    POLISI NJOMBE WAKIRI KUNA SHIDA YA MIGOGORO

    0
    By arushatv on September 19, 2022 Makala

    Na Emmanuel octavian

    Wakati kituo cha sheria na haki za binadamu kikiweka kambi kutoa msaada wa kisheria mkoani Njombe katika maadhimisho ya miaka 27 tangu kuanzishwa kwake mwaka 1995 Jeshi la polisi limekiri kuwapo kwa migogoro mingi na mauaji yanayohitaji msaada wa kisheria toka LHRC.

    Katika ufunguzi wa utoaji wa huduma za msaada wa kisheria yanayofanyika kitaifa mkoani Njombe kupitia kituo hicho kwa muda wa siku 10 kaimu kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Butusyo Mwambelo anasema msaada wa kisheria unahitajika sana kutokana na matatizo lukuki yaliyopo katika jamii.

    Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi mtendaji wa kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC,Wakili Fulgence Massawe ambaye ni mkurugenzi wa uchechemuzi na maboresho wa kituo hicho anasema tayari wamewafikia maelfu ya wananchi wenye matatizo mbalimbali na kuwapa msaada wa kisheria huku wakiadhimisha miaka 27 mkoani Njombe kutokana na utafiti kubaini kuwapo kwa changamoto nyingi katika mikoa ya kusini mwa Tanzania

    Akifungua maadhimisho hayo ya huduma za msaada wa kisheria kwa niaba ya Mkuu wa mkoa wa Njombe,Katibu tawala mkoa Bi.Judica Omary amesema kwa kufanyika maadhimisho hayo mkoani hapa kutawapa fursa wananchi kupata huduma hiyo pasina gharama yoyote kwa maslahi mapana ya familia na taifa kwa ujumla

     

    Mwisho

    Post Views: 56
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleVijiji 20 Longido vyatenga hekta 186.794 kwa ajili ya nyanda za malisho
    Next Article PANYA RODI’ 135 WANASWA DAR ! MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA24TV

    Related Posts

    ASKOFU MASANGWA AKOSHWA NA MCHUNGAJI ALIYETUMIKIA KANISA KWA MIAKA34 AMEACHA ALAMA KUBWA

    February 26, 2023

    MZEE MOLLEL AZIKWA KIJIJINI KWAKE WANANCHI WAMWAGA MACHOZI WAZMIA WAKIAGA MWILI WAKE

    February 7, 2023

    WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amezindua zoezi la ugawaji wa vishikwambi 293400 Kwa walimu wote nchini

    November 5, 2022

    PROFESA KIKULA AAINISHA MIKAKATI YA TUME YA MADINI KWENYE UBORESHAJI WA SEKTA YA MADINI

    October 13, 2022

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.