Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Break News»KARANI WA SENSA AJIFUNGUA KABLA YA ZOEZI LA SENSA DC NASSARI AFUNGUKA ! KUHUSU ZOEZI LA SENSA BUNDA

    KARANI WA SENSA AJIFUNGUA KABLA YA ZOEZI LA SENSA DC NASSARI AFUNGUKA ! KUHUSU ZOEZI LA SENSA BUNDA

    0
    By arushatv on August 24, 2022 Break News

    Na mwandishi wa A24Tv .Musoma.

    Karani wa Sensa ya Watu na Makazi wilayani Bunda mkoa wa Mara amejifungua muda mfupi kabla ya kuanza kazi hiyo, hivyo kulazimika kuondolewa kwenye orodha ya makarani katika wilaya hiyo.

    Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Joshua Nassari amesema kuwa karani huyo amejifungua usiku wa kuamkia Agosti 23, 2022 ingawa hakuweza kumtaja jina

    “Tangu tumeanza tumepata changamoto ambayo pia ni baraka kuna karani wetu amejifungua usiku na bahati nzuri alijifungua kabla ya saa sita kwahiyo yeye na mtoto wake pia wamehesabiwa na baada ya hali hiyo kujitokeza tayari karani wa akiba ameshachukua nafasi na kazi inaendelea,” amesema Nassari.

    Amefafanua kuwa wilaya ya Bunda inao makarani zaidi ya 1,000 na kwamba shughuli ya kuhesabu watu na makazi inaendelea na huku akiamini kuwa kazi hiyo itakamilika kwa ufanisi.

    Amewataka wakazi wa Bunda kutoa ushirikiano kwa makarani na kutoa taarifa sahihi zitakazowiewezesha serikali kupanga mipango ya maendeleo kwa nchi na wananchi kwa ujumla.

    Nassari pia amewataka wakazi wa wilaya hiyo hasa wale ambao bado hawajahesabiwa kuwa watulivu na wavumilivu kwa maelezo kuwa ni lazima kila mtanzania atahesabiwa katika muda ambao tayari umetangazwa.

    “Nimekuwa nikipokea simu kutoka kwa watu wanalalamika kuwa bado hawajafikiwa naomba nitumie nafasi hii   kuwaondoa hofu kwamba lazima kila mtu atafikiwa, ndio kwanza siku ya kwanza imeisha,” amesema.

    Amewataka wakuu wa kaya wilayani humo ambao bado hawajahesabiwa kuendelea na shughuli zao huku wakiwa wameacha taarifa zao na mawasiliano yao nyumbani ili makarani wakifika kwenye kaya zao iwe rahisi kupata taarifa zao.

    Mwisho .

    Post Views: 53
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMREMA KUZIKWA KESHO KIJIJINI KWAKE KIRARACHA ! MAGAZETI YA LEO ARUSHA24TV
    Next Article WAZIRI MKUU MAJALIWA AMLILIA MREMA KUZIKWA LEO ! MAGAZETI YA LEO ARUSHA24TV

    Related Posts

    MKURUGENZI WA JIJI LA ARUSHA AMETOA MILION 33 KUNUNUA UNGA WA LISHE KWA WENYE MAHITAJI MAALUM

    February 9, 2023

    KOREA KUSINI NA CHUO CHA UFUNDI ARUSHA WALETA PIKI PIKI MPYA ZA KUTUMIIA UMEME

    February 5, 2023

    BREAKING NEWS : MUSA JUMA MWENYEKITI MPYA JOWUTA SERIKALI YAAHIDI USHIRIKIANO

    January 29, 2023

    WAFANYA BIASHARA SAMUNGE JIJINI ARUSHA WAPOKEA MILLIONI 100 KUTOKA KWA NABII MKUU GEORDAVIE WAHIDI MAKUBWA KATIKA KUKUZA MITAJI YAO

    January 27, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.