Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»CHUO KIKUU CHA ARUSHA(UOA) CHAWEKA MIKAKATI YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI,KUKUSANYA MIL 50 KILA MWEZI.

    CHUO KIKUU CHA ARUSHA(UOA) CHAWEKA MIKAKATI YA KUJIKWAMUA KIUCHUMI,KUKUSANYA MIL 50 KILA MWEZI.

    0
    By arushatv on July 19, 2022 Habari

    Na Geofrey Stephen Arusha .

    Uongozi wa Chuo Kikuu cha Arusha(UOA) umejipanga kukusanya jumla ya kiasi cha sh,50 milioni kila mwezi kupitia programu ya “Book Project” Kama njia mojawapo ya kujikwamua na changamoto ya kifedha.

    Mbali na programu hiyo pia kimeanzisha miradi mbalimbali ambayo ni ufugaji wa ng’ombe wa maziwa,kuoka mikate,kilimo cha mahindi,pilipili,maharage sanjari na duka kubwa la dawa za binadamu.

    Chuo Hicho ni miongoni mwa vyuo vinavyomilikiwa na kanisa la Waadventista Wasabato nchini ambapo hivi karibuni kilizuiwa na serikali kudahili wanafunzi kutokana na sababu mbalimbali kabla ya kuruhusiwa kudahili wanafunzi mwishoni mwa mwaka huu .

    Akizungumza na waandishi wa habari Naibu makamu mkuu wa chuo hicho kitengo cha mipango, fedha na utawala Prof Nkeni Pearson amesema kwamba Lengo kuu la mradi wa “Book Project” ni kukikwamua chuo chao na changamoto ya kifedha.

    “Tunatarajia hadi kufikia mwezi Septemba kuanza mradi huu ambapo kila mwezi tunatarajia kukusanya milioni 50 hii programu itatusaidia kutukwamua na changamoto ya hali ya kifedha tunayopitia”alisema Prof Pearson

    Hatahivyo,alisisitiza kuwa katika programu hiyo kila muumini wa kanisa la Waadventista nchini atachangia kiasi cha sh,1000 kwa mwezi kupitia nambari ambayo wataitoa hivi karibuni ambapo fedha watakazozikusanya zitawasaidia kulipa mishahara na kuongeza programu mpya.

    “Tuliingia kwenye utawala wa chuo hiki wakati mgumu Sana kwani tulizuiwa kudahili wanafunzi lakini kupitia program hii tunatarajia kila mshirika wa kanisa la waadventista atachangia shilingi elfu moja kwa Mwezi ambayo itatuwezesha kulipa mishahara na kuongeza programu mpya”alisema Prof Nkeni

    Alisema kwamba mbali na kuanzisha programu hiyo pia wanatarajia Kuanzisha kozi ya lugha mbalimbali ambayo ni kichina,kireno,kihispania na kihindi ambapo mitaala hiyo itasaidia kuongeza mapato ya chuo hicho.

    Hatahivyo,mkuu wa chuo hicho,Prof Patrick Mano alisema kuwa wamejipanga katika kipindi cha miaka mitatu ijayo changamoto ya masuala ya kifedha ikiwemo mishahara ya watumishi itakuwa ni historia chuoni hapo.

    Prof Mano ambaye ni raia wa Ghana alisema kuwa hapo awali alipokabidhiwa jukumu la kukisimamia chuo hicho fedha pekee waliyokuwa wakitegemea kuendesha chuo hicho ilitokana na makusanyo ya ada za wanafunzi ambayo haikidhi mahitaji lakini kwa sasa wameweka mikakati kukusanya fedha kupitia miradi mbalimbali.

    Aliitaja baadhi ya miradi hiyo ni pamoja na mradi wa ufugaji wa ng’ombe wa maziwa,kuoka mikate,mradi wa shamba la mahindi,maharage, pilipili ,parachichi sanjari na duka kubwa la dawa za binadamu.

    “Nilipoingia hapa chuoni nilikuta fedha pekee wanayoitegemea kuendesha chuo ni ada za wanafunzi ambayo haitoshi endapo miradi hii ikifanikiwa vizuri suala la mahitaji ya wanafunzi na watumishi litakuwa limemalizika”alisema Prof Mano

    Prof Mano aliomba ushirikino kwa wadau mbalimbali nchini na serikali kusaidia chuo hicho huku akisisitiza ya kwamba miongoni mwa changamoto kuu alizokutana nazo wakati anakabidhiwa majukumu ya kusimamia chuo hicho ni pamoja na masuala ya matumizi mabaya ya fedha za chuo sanjari na changamoto ya utawala bora ambayo kwa sasa imetatuliwa kwa asilimia 70.

    Mwisho.

    Post Views: 255
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleUGONJWA WA HATARI WAGUNDULIKA MAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV
    Next Article MADEREVA 35 BARANI AFRIKA KUCHUANA VIKALI KATIKA MBIO ZA MAGARI ARUSHA

    Related Posts

    Tanzania na India kuendeleza Uhusiano wa Kibiashara na Uwekezaji

    March 27, 2023

    TANZANIA YAKABILIWA NA UHABA WA MABAHARIA VIJANA.

    March 27, 2023

    Marcas Ajitosa kuwania U NEC Arusha

    March 25, 2023

    VIKUNDI 47 KUPATIWA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI MOITA MONDULI

    March 24, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.