Site icon A24TV News

BINTI WA KITANZANIA RAWAN DAKIKI AWEKA HISTORIA NYINGINE KUPANDA MLIMA MKUBWA DUNIANI

Na Mwanfishi wa A24Tv .

Binti wa Kitanzania ,Rawan Dakik mwenye umri wa miaka 22 , mapema wiki hii ameweka rekodi nyingine tena kwa kuwa Mtanzania wa Kwanza Mwafrika kufika katika kilele cha mlima Denali uliopo Bara la Amerika Kaskazini na kuweka historia  ya kupanda vilele saba vya milima mirefu duniani.

“Kilele cha Mlima Denali ulioko Amerika Kaskazini, na kumefanya  jumla ya vilele saba vya juu zaidi duniani vinavyopatikana katika mabara yote saba ya dunia”.

Katikati ya mwaka jana, Dakik alikua Mtanzania wa pili lakini mwanamke wa kwanza Mtanzania na Mwafrika mwenye umri mdogo kufika kilele cha mlima Everest chenye urefu wa mita 8,848, na kuteuliwa kuwa Balozi wa Utalii wa Tanzania.

Hapo awali, Rawan alikuwa tayari amefikia vilele vyote sita vya milima ya dunia na alibaki na mlima Denali pekee, pia inajulikana kama Mlima McKinley, huko Amerika Kaskazini, yenye mwinuko wa kilele wa futi 20,310 (m 6,190) juu ya usawa wa bahari.

Mlima Denali ni kilele cha tatu kwa umaarufu na cha tatu kilichotengwa zaidi Duniani, baada ya Mlima Everest na Aconcagua.

Ipo katika Safu ya Alaska katika eneo la ndani la jimbo la Alaska la Marekani, Denali ni kitovu cha Hifadhi ya Kitaifa ya Denali na Hifadhi.

Milima mingine sita ya kilele kirefu , mwaka 2021 ni pamoja na Mlima Everest iliopo nchini Nepal wenye urefu wa mita 8,848 juu ya usawa wa bahari ambapo aliongoza kwa kufika kileleni.

Mlima mwingine ni Aconcagua, uliopo Argentina wenye urefu wa (m 6,962) alioupanda mwaka mwaka 2018; Mlima Kilimanjaro, Tanzania (5,895) mwaka 2014; Elbrus, Russia (5,642m) mwaka 2016; Vinson Massif, Antaktika (4,892) mwaka wa 2019 na Puncak Jaya, Indonesia, (4,880) mwaka wa 2017

 


Historia hiyo itaijengea heshma kubwa Tanzania kutokana na binti huyo kuitangaza vema duniani baada ya kufanikiwa kuweka historia ya kufika katika vilele saba milima mirefu duniani.

Ends.