Facebook Twitter Instagram
    Facebook Twitter Instagram
    A24TV News
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    A24TV News
    Home»Habari»ASKOFU HOTAY:-AFRIKA INA RASILIMALI NYINGI,IPUNGUZE MISAADA YA NJE.

    ASKOFU HOTAY:-AFRIKA INA RASILIMALI NYINGI,IPUNGUZE MISAADA YA NJE.

    0
    By arushatv on July 31, 2022 Habari

    Na Mwandishi wa A24Tv Arusha .

    Askofu wa kanisa la Anglican Dayosisi ya Mt,Kilimanjaro,Stanley Hotay amesema ya kwamba Afrika ikiwemo Tanzania ina rasilimali za kutosha na kusema ni wakati wa kuwafundisha wananchi kujenga desturi ya kujitegemea.

    Askofu Hotay alitoa kauli hiyo hivi karibuni wakati wa maadhimisho ya miaka 25 ya shirika la Here’s Life Africa Mission zilizofanyika katika kanisa hilo jijini Arusha.

    Sherehe hizo ziliwajumuisha washirika wa makanisa ya kiinjili hapa nchini ,nchi za Afrika Mashariki ,kati pamoja na Afrika Magharibi.

    Akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya sherehe hizo Askofu Hotay ambaye pia ni mkurugenzi wa shirika hilo alisema kuwa lazima waafrika ikiwemo Tanzania wafundishwe umuhimu wa kujitegemea katika kuendesha maisha yao badala ya kutegemea misaada kutoka nje ya nchi.

    “Watu lazima waanze kujifunza kujitegemea tuna rasiliamali nyingi Afrika na Tanzania kwanini tusiwe sisi ndio tunatoa misaada bali kutarajia kwingine?watu wana uwezo wa kujitegemea na kuendesha maisha yao “alisema Askofu Hotay

    Hatahivyo,alisisitiza kwamba katika miaka 25 shirika hilo limefanikiwa kuchimba visima vya maji safi na salama katika baadhi ya nchi za Afrika sanjari na kutoa elimu kuhusu ugonjwa hatari wa Ukimwi barani Afrika.

    Naye mchungaji wa kanisa la Tanganyika African Church (TAC) wilayani Manyoni,Lazaro Mgonde alisema kuwa shirika hilo limemsaidia kukarabati jengo la kanisa analotumia ambalo lilitaka kubomoka.

    “Shirika hilo limenitoa mbali sana maana kuna muda nilitaka kukimbia huduma lakini walinisaidia kuikarabati nyumba ya ibada ambayo ilitaka kubomoka “alisema Mgonde

    Sara Guga ambaye ni mkurugenzi wa shirika la Jesus Glory alisema kuwa wamekuwa wakishirikiana na shirika hilo kuhubiri injili vijijini kupitia mahubiri ya sinema.

    Guga alisema kuwa mbali na kuhubiri pia wamekuwa wakishirikiana kutoa huduma za kiafya kama upimaji wa macho na masikio ambapo wameyafikia maene mbalimbali nchini.

    Mwisho..

    Post Views: 304
    Share. Facebook Twitter Pinterest LinkedIn Tumblr WhatsApp Email
    Previous ArticleMAGAZETI YA LEO NA ARUSHA 24TV
    Next Article VURUGU ZAIBUKA MSIBA WA MATAJIRI ARUSHA,MWANDISHI WA AYOTV ANYANG’ANYWA CAMERA

    Related Posts

    Kamati yapitisha makadirio ya matumizi na maendeleo 2023/2024 kwa Wizara Uwekezaji Viwanda na Biashara.

    March 23, 2023

    MWANDISHI WA HABARI MAARUFU ALLAN ISACK AITAKA NAFASI YA MNEC

    March 23, 2023

    Vyombo vya Dola na wanasheria kushirikiana kutokomeza ujangili Babati

    March 22, 2023

    JIJI LA ARUSHA LATOA MIKOPO YA SHILINGI BILION 2.6 KWA VIJANA WENYE MAITAJI MAALUM NA WANAWEKE

    March 22, 2023

    Leave A Reply Cancel Reply

    Facebook Twitter Instagram Pinterest
    • Home
    • Habari
    • Magazeti
    • Break News
    • Siasa
    • Burudani
    • Makala
    • Michezo
    © 2023 a24tv. Designed by Ishimax Ltd.

    Type above and press Enter to search. Press Esc to cancel.